Sensei Magoma Nyamuko  Sarya
Sensei Magoma, kama anavyojulikana na wanafunzi wake lukuki ndani na nje ya nchi ndiye aliyekuwa gwiji wa Karate na kiungo muhimu kwa sensei Nantambo Camara Bomani (RIP)  katika kuendeleza mwenendo wa Sanaa ya Karate nchini Tanzania. Sensei Magoma (Daudi) amefundisha wanafunzi wengi wa Karate  wa kiTanzania zaidi ya mwalimu yeyote mwingine  hapa nchini. 

Amekuwa mwanafunzi kiongozi  mwenye mamlaka kamili ya kusimamia Dojo lililopo katika shukle ya Msingi ya Zanaki (awali dojo hilo  lilikuwa katika shule ya Sekondari ya wasichana ya Zanaki jijini Dar es salaam na matawi yake yote ya Tanzania tokea mwaka 1976 hadi 1982.

Sensei Magoma ni mmoja kati ya wanafunzi wa tano wa kwanza nchini Tanzania kupata shahada ya kwanza (“Shodan”) mkanda mweusi mwaka 1976 akiwa mwenye umri mdogo kuliko wenzake wote chini ya sensei Bomani. Wanafunzi hao ni: Sensei Mapfumo Gamanya ( Mzibabwe), sensei Tola Sodoinde Malunga, Sensei Abome Mabruki na kaka yake sensei Adombe Mabruki.


Wakati sensei Bomani akiwa huko nchini Marekani kuanzia mwaka 1976 hadi mwaka 1981 sensei Magoma ndiye alikuwa mwanafunzi mkuu kiongozi na mwenye mamlaka yote ya mapendekezo na kutoa test na hata mikanda yote ya mtindo wa Okinawa Goju Ryu Kyokai chini ya mfumo wa kiongozi wao wa Karate duniani Master Eiichi Miyazato, mwalimu wa sensei Bomani. 
Ni vigumu mno kuwataja wanafunzi wote waliopitia chini yake, bali tu, kila mwanafunzi aliyekuwa dojo kwa miaka ya 1976 hadi 1982 alikuwa chini ya himaya yake. Hao ni pamoja na Sensei Rumadha Fundi anayefanya vyema sana huko Marekani, hali kadhalika Edgar Kaliboti ambaye anang'aa nchini Australia. 
Ankal pia alikuwa mmoja wa wanafunzi wa Sensei Magoma kwa miaka kadhaa, na hadi sasa anajivunia uanafunzi wake ambapo haukuwa wa kurusha ngumi na mareke tu, bali pia aliwajenga wanafunzi kifikra na kimwili kwa kuwafunza mazoezi ya hali ya juu ya Yoga.

Licha ya kuwa mkufunzi mkuu wa Karate nchini Tanzania, mara tu baada ya kuondoka kwake mwaka 1982 hapa nchini kuelekea nchi za mashariki ya mbali ikiwemo, India, Nepal, Singapore, Malaysia na Phillipines. Mwalimu Magoma aliacha pengo kubwa sana katika kuimarisha Sanaa ya Karate mtindo wa Goju Ryu nchini Tanzania. Ishukuriwe kwamba wanafunzi wake kadhaa pamoja na wengine waliofuata nyuma yake wanaendeleza sanaa hiyo ya kujilinda kila siku katika dojo la Zanaki, chini ya Sensei Malekia, Sensei Geoffrey Shoo, Sensei Murudker wakisaidiwa na Sensei Almasi na wengineo.

Sensei Magoma pia ni mkufunzi wa Sanaa ya Yoga na mwenye uzoefu mkubwa katika fani hiyo ambayo ilimpeleka nchi nyingi akiwa kama mwalimu na wakati huohuo akifundisha Karate. Alipata mafunzo ya Sanaa ya Yoga nchini India kutoka katika chuo cha “Neo- Humanist Studies” katika mji wa Varanasi, mwaka 1983.

Mengi aliyoyafanya akiwa bado yupo nchini kwa wakati huo, ni pamoja na kutenganisha darasa la mafunzo ya Karate la watoto na watu wazima na kuliita kwa jina ka heshima ya mwanzilishi wa shule hiyo “ Bomani Brigade” au “BB” kama ilivyokuwa anaitwa.

Kundi hilo la vijana wadogoo, lilikuwa halisomi Karate tu, bali pia mwalimu Magoma alijitolea muda wake wote kuwasaidia kimasomo yao kwa “Tuition” ya hisabati, Kiingereza, na kuandika isha mbalimbali zinazohusu maisha kiujumla. Leo hii, ni Zaidi ya miaka takriban  30  na wale vijana wamefaidika sana. Kwa mfano kuna wengi wao kwa hivi sasa ni walimu wa Sanaa ya Karate pia - akiwemo Sensei Rumadha Fundi.

Sensei Magoma, ni mwalimu mwenye upeo wa hali ya juu sana katika Sanaa ya Karate ya Okinawa Goju Ryu Karate-do Jundokan Kyokai na kama nilivyoeleza hapo awali, ameacha pengo kubwa mno ambalo sasa ni dhahiri kwamba kurejea kwake katika kufundisha sanaa hii nchini, kunaweza kuwahamasisha walimu wengi na kuiga mfano wake wa kuwa na moyo na nia ya kusaidia vijana na kuwapa nishani katika maisha yao ya baadae.


Kwa mengine Zaidi yanayohusika na Sensei Magoma na jinsi yakuwasiliana nae yatafuatia hao baadae. 
 Sensei Magoma (fulana ya rangi ya chungwa) akiwa mgeni rasmi katika sherehe za kuadhimisha miaka 37 ya Dojo la Zanako Aprili 20, 2010. Kulia kwake ni Sensei Heri Kivuli
 Sensei Magoma (fulana ya rangi ya chungwa) akilishwea keki na mmoja wa wanafunzi wake Ambaye ni Ankal katika sherehe za kuadhimisha miaka 37 ya Dojo la Zanako Aprili 20, 2010. Kulia kwake ni Sensei Heri Kivuli
Kiongozi mkuu wa Dojo hilo hivi sasa Sensei Malekia akiwa na Japhet Kaseba ambaye pia ni mwanafunzi mwandamizi katika shule hiyo.
Na kupata habari za nyuma kuhusu Goju Ryu Karate nchini Tanzania 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. uncle kumbe na wewe upo fiti. nitakuja kujaribu siku moja km vile putin alipoenda japan akzipiga kidogo.,,,

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...