Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli,Mh Edward Lowassa (watatu kulia) akiwakaribisha Mawaziri wa zamani wa nchini Kenya William ole Ntimama (tai nyekundu) na John Keen (kushoto) nyumbani kwake Monduli. Wanasiasa hao wakongwe na wenye ushawishi mkubwa katika eneo la Maasai Land nchini Kenya walimtembelea Mh. Lowassa ambaye ni Laigwanan Mkuu wa Wamasai wote Afrika Mashariki, na kujadiliana naye masuala mbalimbali lakini zaidi ni juu ya suala la ardhi ambalo limekuwa tatizo kubwa kwa jamii ya wamasai.Wazee hao wanatarajiwa kuhudhuria semina maalum katika jimbo la Monduli wiki ijayo kuzungumzia tatizo la ardhi.Semina iliyoandaliwa na Mh. Lowassa itawashirikisha viongozi wote wa wilaya hiyo pamoja na wakuu wa kimila.Akizungumzia suala la ardhi mzee John Keen alisema mtu anayeuza ardhi anauza utajiri na kununua umasikini.
Home
Unlabelled
Wakongwe wa siasa nchini Kenya wamtembelea Mh. Lowassa Monduli
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...