Meneja uzalishaji wa kampuni ya Nokia Afrika Mashariki, Kingori Gitahi akiwaonesha waandishi wa habari moja kati ya simu tatu zilizozinduliwa.

Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Nokia Afrika Mashariki, Bi.Lilian Nganda akizungumza na waandishi wa habari Septemba 3,2014 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa simu mpya ya Nokia aina ya Lumia 530, 630 na 930.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia tukio la uzinduzi wa simu hizo.
 Kati ya wafanyakazi wa kampuni hiyo wakishuhudia uzinduzi huo jijini Dar es Salaam leo.
Miongoni mwa wafanyakazi wa kampuni hiyo wakishuhudia uzinduzi huo jijini Dar es Salaam leo.HABARI / PICHA NA PHILEMON SOLOMONI

WAFANYABIASHARA na watumiaji wengine wa simu za kiganjani wamepata matumaini mapya baada ya simu nyingine tatu aina ya Nokia Lumia 530, 630 na 930 kuzinduliwa.

Kwa mujibu wa Meneja uzalishaji wa kampuni ya Nokia Afrika Mashariki, Kingori Gitahi akizungumza Dar es Salaam, Septemba 3, 2014  wakati wa kuzindua simu hizo alisema zinauwezo mkubwa kwa matumizi ya mtandao.

"Naamini kwa wafanyuabiashara na watumiaji wa kawaida watakuwa wamepata fursa nzuri ya kutumia na kupkea email kwa urahisi sanjari na kuchukua picha za video na zilizomo katika mitandao kwa wepesi,"alisema.

Pia aliongeza katika kuhakikisha wanatoa huduma nzuri za uhakika wameshirikiana na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Vodacom na Airtel ambao hutoa vifurushi mitandao kwa wateja watakaonunua simu hizo.


Gitahi aliongeza kuwa simu hizo zinauwezo wa kupiga picha kwa haraka zaidi na kurekodi matukio mbaliombali kwa ustadi mkubwa na anaamini watu wengi watakuwa watumiaji wazuri ili kujiweka katika kiwango cha kimataifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...