Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama mbaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASAT) akizungumza katika tamasha la Uimbaji na Uchangiaji wa Ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Segerea jijini Dar es Salaam na kuahidi kutoa sh. milioni 6 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa kanisa hilo. Msama alikuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo akimwakilisha Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Miochezo, Dk. Fenela Mukangala.
 Mchungaji Emmanuel Masanja 'Masanja Mkandamizaji' aliguswa na kutoa ahadi ya shilingi milioni 1 katika hafla hiyo.
 Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la KKKT Usharika wa Tabata Matumbi, Mchungaji Christosiler Kalata akimkabidhi Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama sehemu ya mchango walioahidi katika tamasha la Uimbaji na Uchangiaji wa Ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Segerea jijini Dar es Salaam. Usharika huo ulitoa ahadi ya sh. laki 7.


MJUMBE wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Alex Msama ametoa kitita cha sh. mil 6 katika harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika Segerea.



Msama ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, alitoa kiasi hicho katika harambee hiyo ya kufanikisha ujenzi huo, iliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubelee jijini Dar es Salaam, huku akitoa na ushuhuda wa maisha yake mpaka kufikia hatua aliyofikia sasa.



Akizungumzia ushuhuda huo, Msama aliwataka waumini kuiga mfano wake kwa kujitolea bila ya kugeuka nyuma, kwani ana imani Mungu yupo na anatenda muujiza kama alioutenda kwake.

"Unajua mimi katika maisha yangu hakuna ninayemwamini zaidi ya Bwana Yesu, kwa kuwa bila ya yeye mie nisingekuwa hapa nilipo, kwa taarifa yenu wapendwa mimi nilishakuwa dereva taxi, nilishakuwa kondakta wa daladala, lakini Mungu ni mwema na anatenda muujiza mpaka mimi kuwa hivi," alisema Msama.

Msama ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, aliongeza kuwa hata hivi karibuni katika ajali aliyoipata akienda Dodoma licha ya kupinduka gari mara nne lakini alitoka akiwa hai.

Harambee hiyo iliyoenda sambamba na mnada, ilihudhuriwa na wasanii mbalimbali wa muziki wa Injili kama Masanja Mkandamizaji, Edson Mwasabwite aliyeimba wimbo wa Ni kwa neema tu.

Mbali ya kiasi hicho alichotoa, Msama pia alichangia katika mnada uliofanyika katika tamasha hilo na kununua mtungi wa gesi kwa sh. laki 5.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...