Mfuko wa Maendeleo ya jamii TASAF umeanza kuwajengea uwezo wataalamu ngazi ya Kata kutoka mamlaka nane za utekelezaji wa mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na kuwawezesha walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya masini kuibua miradi inayoweza kutekelezeka ndani ya kipindi kifupi katika mpango wa miradi ya ajira kwa walengwa (Public Works Project kwa lengo la kuwaongezea kipato).

Akifungua warsha ya kuwajengea uwezo wataalamu hao mjini Bagamoyo mkoani Pwani, Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bwana Ladislaus  Mwamanga amesema miradi ya ujenzi itakayoibuliwa na walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini itatekelezwa sambamba na Mpango wa uhawilishaji fedha kwa walengwa jambo litakalosaidia kaya hizo kuongeza  kipato hususan wakati wa kipindi cha hari.

Bw. Mwamanga ameeleza kuwa lengo kuu la mpango huo ni kuhakikisha kuwa wananchi wa Tanzania wanaondokana na umaskini ili waweze kumudu mahitaji yao muhimu kama vile kupata huduma za elimu, afya na lishe.

"Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini haulengi tu katika kuhawilisha fedha kwa walengwa bali pia unahimiza ushiriki wa walengwa katika kazi za mikono kupitia miradi ya mbalimbali katika maeneo yao ili waweze kupata kipato, na kuwekeza" amefafanua Bw. Mwamanga.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa miradi wa TASAF Amadeus Kamagenge amesema Mpango huo ni muhimu kwa vile unatoa fursa ya ajira kwa walengwa katika Kaya Maskini, unawezesha kaya za walengwa kupata kipato zaidi, unawapataia walengwa weledi na stadi za mbalimbali wakati wa utekelezaji miradi, unawezesha jamii husika katika maeneo ya utekelezaji kuweza kuwa na rasilimali kama barabara ambazo hubaki na kuendelea kutumika pamoja na kujenga moyo wa kufanya kazi ili jamii iweze kutoka katika umaskini.

Awali, Mtaalamu wa Mazingira toka TASAF Makao Makuu Bw. Barnabas Jachi alizitaja mamlaka za utekelezaji zitakazoanza kutekeleza mpango huo kuwa ni za Bagamoyo, Kibaha, Chamwino, Mtwara Manispaa, Lindi Manispaa na halmashauri ya wilaya ya Lindi.Warsha hizo zitafanyika katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni mkakati maalum wa TASAF kujenga uwezo wa kitaalamu katika maeneo ya utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini  PSSN.
  Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Ladislaus Mwamanga akifungua warsha ya kuwajengea uwezo wataalamu wa kisekta Mjini Bagamoyo.
 Mkurugenzi wa Miradi wa TASAF Bw. Amadeus Kamagenge akielezea manufaa ya mpango unaotoa fursa ya ajira kwa walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini PSSN kwa lengo la kuwaongezea fursa za kipato.
 Mtaalamu wa Mazingira toka TASAF Makao makuu Barnabas Jachi akitoa maelezo ya awali juu ya warsha ya kuwajengea uwezo wataalamu wa kisekta.



 Picha hii na mbili zinazofuatia ni Washiriki wa Warsha ya kuwajengea uwezo wataalamu wa kisekta (katika makundi tofauti) wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Ladislaus Mwamanga (katikati waliokaa) Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Miradi TASAF Bw. Amadeus Kamagenge

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...