Mtaalamu wa Lishe Tom Mwaipenye kutoka taasisi ya Foot Print, akiwaeleza akina mama waishio maeneo yanayozunguka hospitali ya Halmashauri ya Meru mkoani Arusha, umuhimu wa Virutubishi kwa afya bora ya mwili na akili za mtoto, ikiwa ni sehemu ya kampeni za kuelimisha umma juu ya faida za kutumia Virutubishi ili kuboresha afya. Kampeni hizi zinaendeshwa na serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Taasisi ya Chakula na Lishe, na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania
Akina mama waishio maeneo yanayozunguka hospitali ya Halmashauri ya Meru mkoani Arusha, wakipatiwa elimu ya lishe katika kampeni za matumiziya vyakula vyenye virutubishi zinazoendeshwa na serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Taasisi ya Chakula na Lishe, na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...