Watanzania, Asasi zisizo za serikali na wadau mbalimbali hapa nchini wametakiwa kuwa
mabalozi waLishe Bora katika jamii zinazo wazunguka, hayo yamesemwa na Katibu Mkuu
wa Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii Ndugu Charles A. Pallangyo katika warsha ya siku
3 iliyofunguliwa leo tarehe 23 hadi 25 September 2014 katika Hotel ya Serena jijin Dar es
salaam.
“Serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara yake ya Afya na Taasisi ya Chakula
na Lishe Tanzania imeendelea kuratibu masuala la lishe bora nchini, mfano mwaka 2013
serikali kupitia wizara ya afya imeanzisha kampeni nchi nzima yenye kuhamasisha lishe bora,
na katika kutekeleza Mpango Mkakati wa Lishe Tanzania (National Nutrition Implementation
Plan) e, serikali imeajiri maafisa wa lishe katika Halmashauri takribani 147 na mikoa 20 huku
ikiazimia kufikia halmashauri zote na Mikoa yote Tanzania Bara. Alisema Ndugu Charles A.
Palangyo
Aidha Katibu Mkuu aliweza kuzungumzia changamoto wanazokumbananazo katika
kuhamasisha maswala ya Lishe bora nchini na kuwataka wadau, mashirika na Asasi zisizo za
kiserikali kuendelea na mkakati huo.
“Pamoja na jitihada tunazozifanya , bado kuna changamoto katika zoezi zima la kuboresha
lishe kwa watanzania, kwa mfano asilimia 42 ya watoto chini ya umri wa miaka 5 wamedumaa,
asilimia 16 ya watoto hao wanaukondefu , na watoto wanaozaliwa na uzito pungufu wanakaribia
kuwa asilimia 21.
Ukiachalia hilo, kwa upande wa kina mama, inakadiriwa kuwa asilimia 11 huwa wanakuwa
na uzito pungufu, huku 53% ya wajawazito wanakumbwa na tatizo la upungufu wa wekundu
wa damu. “Hivyo ningependa kuwaomba wadau, mashirika yaliyo bega kwa bega na serikali
yaendelee kujitolea katika safari hii ya kuhakikisha kila mtanzania anapata lishe bora”,
Aliongeza katibu mkuu Charles A. Palangyo.
Warsha hiyo ya kuhamasisha lishe bora katika jamii za kitanzania imefunguliwa leo na katibu
mkuu wa wizara ya afya na ustwahi wa jamii katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam huku
ikitazamiwa kufikia tamati tarehe 25 Septemba 2014.
Waratibu wa warsha hiyo ni shirikisho la SUN Movement Secretariat ambalo ni jumuhisho
la nchi hamsini na nne (54) waliodhamiria kuboresha masuala ya lishe ndani ya jamii zao,
ikishrikiana na Serikali ya Tanzania, PANITA pamoja na World Vision. Warsha hii inawashiriki
kutoka nchi tisa Africa ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Nigeria, Zambia, Zimbabwe,
Mozambique, Malawi na Tanzania
Mgeni Rasmi,Ndg. Charles A.Pallangyo akiwahutubia wageni waliofika katika warsha hiyo serena hotel.
Mkurugenzi Mtendaji PANITA, Ndg. Tumain Mikindo akitoa nasaha zake kwa washiriki.
Mheshimiwa Mbunge Lediana Mafuru Mungo'ng'o akielezea nafasi yake katika masuala ya lishe bora.
Ndg. Brenda kaijuka , mshauri kutoka SUN akiwaelezea washiriki namna ya kuhamasisha lishe bora.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...