Kampuni ya African Barrick Gold (ABG) imesaini mkataba wa miaka miwili (MoU) na Chuo Kikuu cha Afya cha Muhimbili (MUHAS) idara ya Mazingira na Afya bora kazini(Environmental and Occupational Health Sciences) ili kuboresha taluma za madaktari.

Ushirikiano huu utawezesha wanafunzi wa idara hiyo kupata nafasi za kwenda kufanya masomo kwa vitendo yani (field practise) kwenye ofisi na migodi ya kampuni ya ABG, pia pesa hizo zitatumika kwenye kukarabati majendo na utoaji wa vifaa mbalimbali vya maabara na utafiti kwenye kitivo hiyo ya Mazingira na Afya bora kazini.

Mkataba huu unathamani ya zaidi ya shilingi za Kitanzania milioni 300jiwa kuanzisha mfumo maalumu wa kuwasaidia wanafunzi wa kitivo cha Mazingira na Afya Kazini, kwa lengo la kuimarisha maarifa ya wahitimu wenye mafunzo ya vitendo.

Akizungumza katika tukio hilo, Bw,Deo Mwanyika: Makamu wa Rais Shughuli za Ofisi: amesema "Kwa miaka miwili iliyopita ABG, imekuwa ikushirikiana na MUHAS ili kusaidia na kuboresha ujuzi wa wanafunzi na wafanyakazi kwa lengo la kukuza na kuendeleza wataalamu wenye vipaji.

Makubaliano haya tunayo saini leo yatawapa nafasi wanafunzi bora 20 kupata misaada ya kifedha kwa miaka miwili ijayo. Zaidi ya hayo wanafunzi watapata fursa za kufanya mafunzo kwa vitendo kwenye migodi yetu kupitia mpango huu".

Sisi kama ABG,tutaendelea kufanya kazi na taasisi nyingine ili kutafuta ufumbuzi wa uhaba wa wataalamu wenye ujuzi wa madini kwa usimamizi bora wa sekta ya madini Tanzania.

Na kama sehemu ya Chama cha Madini na Nishati Tanzania (TCME) na Mpango maendeleo ya ujuzi, ABG na wadau wengine ambao ambao wanatoa Mafunzo ya Ufundi (IMTT) ya muda mrefu ili kukidhi mahitaji ya haraka ya sekta ya madini inayokua haraka.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Sayansi ya Afya cha Muhimbili (MUHAS) Prof. Ephata Kaaya (kushoto) akiwa na Makamu wa Rais wa shughuli za Ofisi wa African Barrick gold,Deo Mwanyika Wakitiliana saini ya makubalino ya miaka miwili ambapo kampuni ya ABG imetoa zaidi ya TSH 300 ili kusaidia wanafunzi na wafanyakazi wa MUHAS kitivo cha Mazingira na Sanyansi ya Afya bora Makazini, makubaliano hayo pia yatasaidia wanafunzi kupata nafasi za kufanya mazoezi ya vitendo kwenye migodi ya ABG, na vilevile kukarabati majengo, ada za wanafunzi bora,kununua vifaa vya maabara na kutenga fungu la kufanya utafiti.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Sayansi ya Afya cha Muhimbili (MUHAS) Prof. Ephata Kaaya (kushoto) akiwa na Makamu wa Rais wa shughuli za Ofisi wa African Barrick gold,Deo Mwanyika Wakibadilisha mikataba baada ya kutiliana saini makubalino ya miaka miwili ambapo kampuni ya ABG imetoa zaidi ya TSH 300 ili kusaidia wanafunzi na wafanyakazi wa MUHAS kitivo cha Mazingira na Sanyansi ya Afya bora Makazini, makubaliano hayo pia yatasaidia wanafunzi kupata nafasi za kufanya mazoezi ya vitendo kwenye migodi ya ABG, na vilevile kukarabati majengo, ada za wanafunzi bora,kununua vifaa vya maabara na kutenga fungu la kufanya utafiti.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...