Kampuni ya simu za Mkononi ya Bharti Airtel yenye kufanya shughuli zake katika nchi 20 barani Afrika na Asia leo imetangaza mpango wa kuzindua huduma ya kutuma na kupokea pesa Afrika Mashariki. 
Huduma hii ya kwanza barani Afrika itamwezesha Mteja wa Airtel kutuma , kupokea na kutoa pesa kutoka kwenye salio lake la Airtel Money Hatua ya awali ya huduma hii inategemea kuanza tarehe 1 November 2014 kwa kushirikisha nchi za Kenya, Uganda, Tanzania na Rwanda ambapo huduma hii itaweza kupatikana kufatia kibali kutoka benki kuu ya serikali ya Rwanda, Kenya, Tanzania na Uganda cha kuendelea na uzinduzi wa mpango huu. 

Hatua ya pili ya mwendelezo wa mpango huu kwa nchi nyingine za Afrika ambapo Airtel inaendesha biashara yake zinategemea kuanza mwakani. Akiongea wakati wa Mkutano wa Biashara kwa wakuu wa Makampuni katika nchi za Afrika Mashariki uliyofanyika Rwanda, Mkurugenzi na Mkuu wa kitengo cha Airtel Money bw, Chidi Okpala,alisema” hii ni hatua muhimu itakayowawezesha wateja wetu kuondoa vikwazo vya kutuma na kupokesa pesa nje ya mipaka ya nchi zao kiurahisi kuweza kufanya hivyo kwa kupitia huduma ya Airtel Money. 

Huduma hii itatanua wigo, kutoa unafuu na kuleta urahisi kwa wafanyabiashara wadogo kufanya malipo ndani na nje ya mipaka ya nchi za Afrika Mashariki.” Aliongeza kwa kusema “huduma hii pia italeta fulsa za kibiashara, ni wazi kwamba huduma za kifedha kupitia simu ni muhimili mkuu katika ushirikiano wa huduma za kifedha na ndio dhamira ya serikali za Rwanda, Uganda, Kenya na Tanzania katika kuhakikisha inakuza shughuli za kibiashara ndani ya nchi za Afrika Mashariki.” Sambamba na hilo Hatua hii ya kwanza ya uzinduzi wa huduma hii pia itawawezesha wateja wa Benki ya Afrika nchini Kenya na Uganda kutuma na kupokea pesa katika nchi hizi mbili. 

 Huduma ya Airtel money ni huduma ya kifedha kupitia simu ya mkononi iliyo salama na rahisi inayowawezesha wateja kutuma pesa kutoka simu moja kwenda kwenye simu za mitandao yote, pia inamuwezesha mteja kununua muda wa maongezi kwaajili ya simu yake au kwa simu ya mtu mwingine. 

Pia inawawezesha wateja kulipa ankra zao mbalimbali na kutoa pesa katika mashine za (ATM)’s Imekaririwa na jumuiya ya Afrika Masharika kwamba huduma za kifedha kupitia simu za mkononi ni muhimu katika nchi hizi kutokana na urahisi, uharaka na inaokoa muda kwa wateja na wafanyabiashara. Uzinduzi wa huduma za kibunifu kama vile za mikopo, kuweka pesa, na kutoa huduma za bima zinazofanywa kwa kushirikiana na makampuni yanayotoa huduma za kibenki zimeleta mabadiliko chanya na kuongeza kasi ya ushirikiano wa kuvuka mipaka ya nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...