Mkuu wa Wilaya ya
Mbeya mjini Dr. Norman Sigela(mwenye suti nyeusi)pamoja na Mchezaji bora wa
Mwezi wa Septemba wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara Anthony Matogolo wa timu
ya Mbeya City(kushoto)wakionesha hundi yenye thamani ya Tsh Milioni 1/= kwa
mashabiki wa timu yake mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Mkuu wa wilaya hiyo kwa niaba ya wadhamini
wakuu wa ligi kuu Vodacom Tanzania hapo jana kabla ya mechi kuanza baina ya
timu Mbeya City na Azam FC,Ambapo Azam
FC iliilaza Mbeya City kwa goli moja bila na anaeshuhudia kulia ni Katibu wa
chama cha mpira wa miguu mkoa wa Mbeya(MREFU) Seleman Harub.
Mchezaji bora wa Mwezi wa Septemba wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara Anthony Matogolo wa timu ya Mbeya City akionesha kikombe chake
mtanange ukiendelea katika ligi kuu ya vodakom katika
uwanja wa sokoine
Wachezaji wa timu ya Azam
FC wakishangilia goli lao lililofungwa na Aggrey Morris katika mzunguko wa Ligi kuu ya
Vodacom Tanzania bara kati ya timu hiyo na Mbeya City hapo jana/juzi Azam FC
iliilaza Mbeya City kwa goli 1-0.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...