Wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango
wakiangalia chanzo cha chemichemi ya maji cha Ikorongo kilichoko kilometa 13.2
kutoka Mpanda mjini. Chanzo hicho kina uwezo wa kutoa maji ya kutosha mji wote
wa Mpanda.
Mhandisi wa Maji wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda Magdalena Mkeremi
(aliyejifunika mtandio) akifafanua jambo kwa timu ya wakaguzi wa miradi ya
maendeleo kutoka Ofisi Rais, Tume ya Mipango walipotembelea chanzo hicho hivi
karibuni
Mhandisi
Happiness Magalula, Naibu Katibu Mtendaji anayesimamia Klasta ya Miundombinu na
Huduma (mwenye sweta la blue) akitaka ufafanuzi wa miundombinu ya kuwezesha
maji kuwafikia wananchi kutoka katika chanzo hicho. Bomba la inchi kumi
limetandazwa kutoka kwenye chanzo hicho mpaka mjini ambako kuna tanki kubwa la
maji yanayosambazwa katika mji wa Mpanda na vitongoji vyake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...