Jumuiya ya wa-Islam wanaozungumza ki-Swahili ktk mji wa Coventry uliopo nchini Uingereza (United Kingdom), wameadhimisha swala ya Eidil hajj kwa mafaniko makubwa. 
Pamoja na mambo mengine waliandaa sherehe za Eid ambazo ziliendelea kwa muda wa siku mbili mfulilizo Jumamosi 4/10/2014 na  Jumapili 5/10/2014 ambapo vyakula vya kiasili vitaandaliwa. 
Sherehe hizo pamoja na mambo mengine  zina malengo ya kuzikusanya pamoja familia kwa ajili ya kujenga jamii yenye nguvu na yenye kuhimizana maadili mema. 
Malengo hasa ya jumuiya ni kuhakikisha kua jamii inakua pamoja kwani kwa kufanya hivyo inaamini kwamba itapatikana fursa ya kuwafundisha watoto na watu wazima malezi bora ikiwa ni pamoja na kuifahamu vizuri dini yao, utamaduni wao na kuhimizana mambo mema ambayo ulimwengu mzima unahangaika kuhakikisha kwamba, dunia inakua ni mahali pa amani na utulivu. 
Kwa ajili ya kuifahamu zaidi COMSWA na malengo yake tembelea http://www.comswa.com/

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...