Mwanadada Laveda kutoka Tanzania akilakiwa kwa shangwe alipoingia ndani ya jumba la Big Brother Africa Hotshots usiku wa leo baada ya kushinda kwa kura nyingi sana shindano la vipaji ambapo kila mshiriki alipewa nafasi ya dakika tatu kuonesha kipaji chake. Laveda aliingia na Saxophone na kufurahisha kadamnasi kwa umahiri wake na hatimaye akapewa cheo cha kiongozi wa nyumba wa kwanza katika onesho hili kwa mwaka huu.
Laveda akipuliza saxophone kwa umahiri mkubwa uliompa kura kibao usiku huu. Yaani hapa hata King Maluu atapiga saluti...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Good...............
    mm....mmm ..mmm...lakini.... mbona kama rangi za bangiri alizovaa mkononi huyu anayeitwa mwakilishi wa hii nchi nzuri, ukizitazama kwa makini na kwa ujumla wake unapata taswira ya bendera ya nchi fulani ya EAC?
    Naomba nielimishwe vema, maana kuuliza ni moja ya kukuza ufahamu au maarifa.

    Mzalendo


    ReplyDelete
  2. Hongera kwa mrembo. Kwakweli mwanzo wake ni mzuri. Kazi iko kwa kaka mwakilishi wetu. Jamani yeye lengo lake kwenda Big Brother ni si lingine ila ni totoz. Yaani yeye hata ushindi hauwazii... kha!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...