Mkuu wa idara ya data na vifaa vinavyotumia intarnet kutoka Tigo, David Zacharia akielezea wateja watakavyotumia huduma hiyo kwa urahisi,mbele ya Wanahabari jijini Dar leo.

 Mkuu wa ukuaji na ushirikiano wa mitandao ya kijamii kutoka Tigo, Naheed Hirji, akielezea upatikanaji wa huduma hiyo.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria hafla hiyo.

KAMPUNI ya mtandao wa Tigo, imetangaza rasmi ushirikiano kati yao na mtandao wa kijamii wa Facebook ambapo itatoa ofa ya Intaneti itakayotumiwa kwa bei nafuu kupitia ‘application’ maalum ya Intaneti Organisation.

Tigo pia inatoa fursa ya wateja kununua simu za kisasa ‘smartphones’ kwa bei nafuu, ili kupata huduma bora ya intaneti na  tovuti za huduma  kama vile elimu, afya, habari na mitandao ya kimawasiliano zitakazopatikana bila malipo

Akizungumza na kwenye mkutano na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar, mkuu wa idara ya data na vifaa vinavyotumia intaneti kutoka Tigo, David Zacharia, alisema ushirikiano wao na Facebook utaongeza matumizi ya tekinolojia ya kidijitali nchini kwa Watanzania wengi kutumia mtandao wa intaneti.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...