Bondia Francis Miyeyusho (kushoto)  akitunishiana misuli na Emilio Norfat ambao watazipiga kesho Jumapili October  5 katika uwanja wa Mkwakwani Tanga mpambano wa raundi nane.
--------------------------------------------  
 MABONDIA mbalimbali watazipiga siku ya Jumapili kwa ajili ya mpambano wa ubingwa ambapo bondia kutoka mkoa wa Tanga Tanzania Alen Kamote 'Rasta'' atazipiga na Osgood Kayuni wa Malawi kugombea ubingwa wa Dunia wa UBO kg 61.
Hiyo ndio siku ya kufurahia kwa wakazi wa Tanga kwani mpambano huo pia uatasindikizwa na mapambano mengine ambapo bondia wa Dar es salaam Thomas Mashali atavaana na bondia kutoka Moshi Alibaba Ramadhani kugombania ubingwa wa Africa wa UBO kg 72 
Pia siku hiyo kutakuwa na mpambano mwingine  mkali kati ya bondia namba moja kwa ubora katika uzito wake featherweight  Fransic Miyayusho atakaezipiga naEmilio Norfat ambaye nae ni namba mbili katika uzito huo

Mapambano hayo yaliyoandaliwa jijini Tanga na promota mkongwe nchini Ally Mwazoa ambaye kwa hivi sasa analeta burudani ya masumbwi nchini kupitia Mwanzoa Promotion

Siku hiyo pia kutakuwa zikiuzwa DVD mpya za masumbwi ambazo zinaonesha mafunzo mbalimbali ya mchezo wa ngumi yanavyoanza hatua kwa hatua mpaka kujua kitu kamili katika mchezo huo pia kunakuwa na mapambano ya mabondia mabigwa wa dunia wa mchezo huo kama Floyd Maywether, Manny Paquaio,mike Tyson, Mohamed Alli pamoja na mabambano ya ngumi ya ndani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...