Mtendaji Mkuu kutoka Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Miradi (PDB) inayoratibu Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), Bw. Omari Issa akiwapa changamoto leo Alhamisi Wakuu wa Mikoa na Wilaya (hawapo pichani) kufanya uamuzi wa haraka katika utekelezaji wa majukumu yao na kutosubiri mpaka wafuatiliwe.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatuma Mwasa na viongozi wengine wakifuatilia hotuba ya Mtendaji Mkuu wa PDB, Bw. Omari Issa mjini Dodoma leo Alhamisi aliyekuwa akiwakumbusha watendaji hao waandamizi umuhimu wa kuchukua uamuzi kwa haraka na kutosubiri kufuatiliwa katika mambo ambayo yamo ndani ya uwezo wao.
Baadhi ya Wakuu wa Mikoa, Wilaya na watendaji waandamizi waliohudhuria Semina iliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Mtendaji Mkuu wa PDB, Bw. Omari Issa (hayupo pichani) alipokuwa akitoa mada kuhusu uwajibikaji mjini Dodoma leo Alhamisi.
Mtendaji Mkuu wa PDB, Bw. Omari Issa akijadiliana jambo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecki Sadiq walipokutana leo Alhamisi mjini Dodoma wakati wa semina inayoendelea kwa Wakuu wa Mikoa, Wilaya na maofisa waandamizi. (Picha zote kwa Hisani ya Ofisi ya Rais-PDB).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Wametoka mbali! Nawakumbuka walipokuwa wote Omari Issa na Said Mecki Sadiq)walikuwa darasa moja hapo Bwiru - darasa la tisa mpaka 12.

    BAP

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...