Mahakama ya hakimu mkazi Kinondoni jijini Dar es Salaam imezuia kufanyika
kwa tamasha lililopewa jina ‘Bang Bang Bear Fest’ lililokuwa linatarajiwa
kufanyika Jumamosi hii.
Uamuzi wa mahakama hiyo umetokana na malalamiko yaliyotolewa na Bongo5
Media Group ambao wanamiliki wazo halisi la tamasha la aina hiyo liitwalo
Dar es Salaam Bear Fest.
Kwa hali hiyo mahakama hiyo imetoa amri ya kusitishwa mara moja kwa ‘Bang
Bang Bear Fest’ lililokuwa lifanyike October 4 kwenye viwanja vya Posta
Kijitonyama, Dar es Salaam pamoja na kulipa hasara yoyote iliyotokana na
kuingiliwa kwa haki miliki hiyo.
Gharama za ku - copy na kupaste bila kuchanganya na akili zako kidogo
ReplyDelete