Mshambuliaji wa timu ya Taifa Stars,Juma Luizio akiipachikia bao nne timu yake katika mtangange wa kikataifa wa kirafiki dhidi ya Benin,uliomalizika hivi punde katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Taifa Stars imeshinda 4-1 dhidi ya Benin.
Wachezaji wa Taifa Stars,wakishangilia ushindi wao huku wakiwaacha wapinzani wao wa Benin wakiwa hoi tena wakiwa hawaamini wanachokiona uwanjani hapo.
Washabiki wa Taifa stars wakiisapoti vilivyo timu yao.
Ubao wa ulionyesha hivi kabla jamaa hawajapata la kufutia machozi.
Shangwe tupu ilikuwa uwanjani hapa.
Dogo muokota mipira akiisikilizia baridi iliyoambatana na kimvua cha kiaina.
Uzalendo ndio mpango mzima,pamoja na kwamba mvua ilikuwa ikinyesha lakini hakuna alietaka kuondoka uwanjani hapo hasa kutokana na burudani safi iliyoonyeshwa na Taifa Stars leo.Picha na Othman Michuzi.,MMG.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...