Baadhi ya washiriki wa warsha ya kujengewa uelewa wa mpango wa kunusureu kaya maskini  unaoratibiwa na TASAF wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa TASAF kwenye ukumbi wa TEC mjini DSM.


Mkurugenzi wa Uratibu wa TASAF,Bw. Alphonce Kyariga (aliyesimama) akifungua warsha ya kuwajengea uelewa kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Ladislaus Mwamanga maafisa ufuatiliaji TA  wa mamlaka za utekelezaji  PAAs kwa pya kwenye ukumbi wa TEC mjini DSM.
  Baadhi ya washiriki wa warsha ya kujengewa uelewa wa mpango wa kunusureu kaya maskini  unaoratibiwa na TASAF wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa TASAF kwenye ukumbi wa TEC mjini DSM.

 Washiriki wa warsha ya siku mbili ya kujengewa uelewa wa Mpango wa  kunusuru kaya maskini  unaoratibiowa na TASAF wakiwa katika ukumbi wa TEC mjini DSM  kupata maelezo ya mpango huo kabla ya kwenye katika maeneo ya utekelezaji  katika mikoa ya Morogoro, Tanga, Mwanza, Shinyanga Na Simiyu.

 Mmoja wa wawezeshaji wa warsha ya kujen gewa uelewa maafisa ufuatiliaji wapya wa mpango wa kunusuru kaya maskini  PSSN  Bi.Woisso  kwenye ukumbi wa TEC mjini DSM .

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF unaanza awamu ya nne (wave 4) ya zoezi la kubaini  kaya maskini katika mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Morogoro, Tanga na Pwani Oktoba 6 Mwaka huu.

Katika maandalizi hayo TASAF imeanza warsha kwa ajili ya wawezeshaji wa Kitaifa, wataalamu wa ufuatiliaji TAs na watumishi wa makao makuu (TMU) ambao watakwenda kufanya kazi kwenye maeneo ya utekelezaji wa Mradi katika mikoa hiyo.

Akifungua warsha  hiyo kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji wa TASAF  Ladislaus Mwamanga, Mkurugenzi wa uratibu wa TASAF  Bw. Alphonce Kyariga amesema kazi ya utambuzi wa kaya maskini ni nyeti na inayotakiwa kufanywa kwa umakini mkubwa ili kupunguza uwezekano wa kutozibaini kaya za walengwa.




Amessistiza kuwa miongozo na taratibu zilizowekwa na TASAF zinapaswa kufuatwa  ili hatimaye zoezi hilo liwe la mafanikio makubwa kama inavyotarajiwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...