Meneja Mradi Uboreshaji wa Uzazi Salama wa Chama cha Wakunga Tanzania (Tama), Martha Rimoy, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo, wakati Taasisi ya Amref Health Africa, ilipokuwa ikielezea kuhusu kuandaa hafla ya chakula cha jioni, Oktoba 9 kwenye Hoteli ya Serena, kwa ajili ya kuchangisha fedha za kufundishia wakunga ili kuokoa afya ya mama na mtoto, katika kampeni ijulikanayo kama 'Stand up for African Mother'. Wengine pichani ni Mkurugenzi Mkazi wa taasisi hiyo, Dk. Festus Iloko, Naibu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benk M, wafadhili wa kampeni hiyo, Jacquelin Woiso na Naibu Mkurugenzi wa Amref Health Africa Tanzania, Dk. Rita Noronha.
Mkurugenzi Mkazi wa Amref Africa nchini, Dk. Festus Iloko, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo, kuhusu hafla ya chakula cha jioni, itakayofanyika Oktoba 9 kwenye Hoteli ya Serena, ili kuchangisha fedha za kufundishia wakunga kwa ajili afya ya mama na mtoto, katika kampeni ijulikanayo kama 'Stand up for African Mother'. Kulia ni Naibu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benk M, mmoja wa wafadhili wa kampeni hiyo, Jacquelin Woiso.
Naibu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benk M, mmoja wa wafadhili wa kampeni hiyo, Jacquelin Woiso, akifafanua jambo kwenye mkutano huo.
Naibu Mkurugenzi wa Amref Health Africa Tanzania, Dk. Rita Noronha, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari, wakati wa mkutano huo.Picha na Kassim Mbarouk.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...