Na Georgina Misama-MAELEZO 

 Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) imeiwezesha Serikali kukusanya mrabaha wa jumla ya shilingi billioni 5.2 tangu kuanzishwa kwa wakala huo.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi uzalishaji na usafirishaji wa madini Bwn Conrad Mtui wakati wa ziara ya waandishi wa habari walipotembelea migodi ya Lugoba na Msolwa Chalinze, hivi karibuni.

“Wakala umefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi bilioni 5.2 kutokana na madini hayo yaliyozalishwa na kuuzwa na wamiliki halali wa leseni katika mikoa mbalimbali kwenye kanda za Kaskazini, kati, Kusini, Kusini Maghalibi, Maghalibi, Mashariki na Ziwa Victoria” alisema Mtui.

Aidha,Wakala kwa kushirikiana na Ofisi za Madini ulibuni matumizi ya “Hati ya Mauzo” kwa lengo la kudhibiti shughuli za uzalishaji na mauzo ya madini, mkakati ambao ulianza kutumika mwezi Juni, 2011 utakaohusisha Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

Pia, Wakala ulifanya ukaguzi na uhakiki wa madini yaliyozalishwa na kuuzwa na migodi mikubwa ya madini nchini, ikiwa na lengo la kupata mrabaha na takwimu sahihi za madini yaliyozalishwa na migodi hiyo.

Akitaja migodi iliyofanyiwa ukaguzi alisema ni Mgodi wa dhahabu wa Geita, Golden Pride, Bulyanhulu, Tulawaka, North Mara, Buzwagi na New Luika iliyowezesha kukusanywa kwa jumla ya Dola za Marekani milioni 427.98 Akizungumzia kuhusu hatua wanazochukuliwa baadhi ya wamiliki wa migodi wanaokiuka taratibu za “Hati ya Mauzo” Mkaguzi wa Madini ya Ujenzi na Viwandani Abubakari Jihango alisema kuwa hadi sasa kuna kuna kesi 53 mahakamani, na kama itadhihirika ukiukwaji wa sheria, taratibu za kisheria zitafuatwa.
Meneja wa Maabara kutoka Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA) Mhandisi Mvunilwa Mwarabu akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) mashine ya kupimia kiwango cha madini inayoitwa Atomic Absorption Spectroscopy (AAS) walipotembelea Maabara ya Wakala huo jijini Dar es Salaam leo.
Mkemia Alfred Aloyce kutoka Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA) akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) sampuli ya jiwe la dhahabu iliyotayarishwa kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa kimaabara ili kubaini kiasi cha madini ya dhahabu kwenye jiwe hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...