Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group,
Bw. Farough Baghozah (wapili kushoto)akimkabidhi hundi ya shilingi
milioni 13 Mratibu wa Mbio za Rock City Marathon 2014, Bw. Mathew Kasonta (wa
kwanza kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika jijini Dar es Salaam
jana. Mbio hizo zitafanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe
26 Mwezi huu. Wakishuhudia wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN
Group Bi. Pamela Mandari, na Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi.
Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto).
Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.
Farough Baghozah (wapili kulia)akifafanua jambo kwa waandishi
wa habari wakati wa kukabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13
iliyotolewa na kampuni hiyo kudhamini mbio za Rock City Marathon 2014
zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu.
Wakishuhudia kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari,
Mratibu wa mbio hizo, Bw. Mathew Kasonta (wapili kushoto) na Afisa Uhusiano na
Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto).
Mratibu wa mbio za Rock City Marathon,
Bw. Mathew Kasonta, (wa pili kushoto) akiongea na waandishi muda mfupi kaba ya
kupokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13 iliyotolewa na kampuni ya
TSN Group kuoitia kinywaji chake cha Chili Willy kama udhamini wa mbio hizo kwa
mwaka huu zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26
Mwezi huu. Kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw. Farough
Baghozah akifuatiwa na Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela
Mandari, na kushoto ni Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya
Kibanga (wa kwanza kushoto).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...