Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.  Farough Baghozah (wapili kushoto)akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 13 Mratibu wa Mbio za Rock City Marathon 2014, Bw. Mathew Kasonta (wa kwanza kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Mbio hizo zitafanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu. Wakishuhudia wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari, na Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto). 
 Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.  Farough Baghozah  (wapili kulia)akifafanua jambo  kwa waandishi wa habari wakati wa kukabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13 iliyotolewa na kampuni hiyo kudhamini mbio za Rock City Marathon 2014 zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu. Wakishuhudia kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari, Mratibu wa mbio hizo, Bw. Mathew Kasonta (wapili kushoto) na Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto). 
 Mratibu wa mbio za Rock City Marathon, Bw. Mathew Kasonta, (wa pili kushoto) akiongea na waandishi muda mfupi kaba ya kupokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13 iliyotolewa na kampuni ya TSN Group kuoitia kinywaji chake cha Chili Willy kama udhamini wa mbio hizo kwa mwaka huu zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu. Kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.  Farough Baghozah akifuatiwa na Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari, na kushoto ni Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto). 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...