Mkuu
wa Wilaya ya Uvinza Mwalimu Hadijah Nyembo (kulia) akitoa nasaha zake
kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali
Mstaafu Issa Machibya (wa pili kulia) kuzungumza na wakazi wa wilaya ya
Uvinza kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo cha redio jamii Uvinza FM
mkoani Kigoma. Kutoka kushoto ni Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel
Tanzania, Hawa Bayumi, Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa
Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambao ndio wadhamini
wakuu wa redio Uvinza FM, Bi. Rose Haji Mwalimu na Mkurugenzi Mtendaji
wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya.(Picha na Zainul Mzige wa MOblog).
Na Mwandishi wetu, Uvinza - Kigoma
Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya amesisitiza
uadilifu katika vyombo vya habari jamii kwa kutangaza habari zisizoumiza
hisia kwa wananchi wengine na kuepuka migogoro.
Akizindua
kituo cha redio jamii cha Uvinza FM, Luteni Kanali Mstaafu Machibya
alisema kuwa vyombo vina wakati mgumu hasa katika kipindi cha kuelekea
uchaguzi mkuu mwaka 2015.
“Changamoto hii inaweza kuepukika kwa kuhakikisha habari zinazotolewa
zinalenga kuendeleza utamaduni wa amani, upendo, utulivu na uvumilivu na
kuepuka viashiria vinavyoweza kusambaza chuki kwa lengo la kufanikisha
chaguzi salama.
Mkuu
wa Mkoa huyo amesisitiza umuhimu wa kuutumia uhuru wa kutoa na kupata
habari vizuri kwa kusema kwamba uhuru huo usitumike kutoa habari
zinazopendelea upande mmoja na kukandamiza mwingine kwa kuwa hali kama
hiyo husababisha machafuko.
“Kwa
mujibu wa Ibara ya 18 (b) ya Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania
ya mwaka 1977, kila mtu anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari
bila ya kujali mipaka ya nchi, lakini haki hiyo iende sambamba kwa
kuzingatia Sheria za nchi na kuhakikisha habari hizo haziumizi hisia za
wananchi wengine,”
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akisoma
risala wakati wa uzinduzi wa kituo cha redio jamii Uvinza FM ambapo
alilipongeza shirika la UNESCO kwa juhudi kuwaweka karibu wananchi na
serikali kupitia mawasiliano ya redio.
Luteni
Kanali Mstaafu Issa Machibya ameitaka redio jamii Uvinza kuonyesha
uwezo wao ili waweze kujitangaza na kujijengea imani kwa wanajamii wao
kuwa wanaweza. “Ni kwa hali hiyo tu mtaweza kujulikana, kutambulika na
kupata udhamini na matangazo ya kutosha.”
Amewataka
wanajamii kukitumia vyema kituo chao cha redio ili kiwe chachu ya
kuleta na kukuza maendeleo katika vijiji, wilaya, mkoa na taifa kwa
ujumla.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...