Mhariri wa Gazeti ya Citizen la hapa nchini,Bw. Richard Mbamba ambaye ni mmoja kati wanahabari waliowahi kushinda tuzo za "CNN MultiChoice African Journalist of the Year 2008" akisisitiza jambo wakati wa Semina ya simu moja kwa wanahabari wa Tanzania juu ya namna wanavyopaswa kufanya kazi zao,iliyofanyika leo katika Hoteli ya New Afrika,jijini Dar es Salaam.Semina hiyo imekuja ikiwa ni siku moja kabla ya kufanyika wa shughuli ya utoaji tuzo hizo za "CNN MultiChoice African Journalist of the Year 2014" itakayofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar es Salaam Oktoba 18.PICHA NA OTHMAN MICHUZI.
Mhariri wa Gazeti la City Press la nchini Afrika Kusini,Ferial Haffajee akizungumza wakati wa Semina ya simu moja kwa wanahabari wa Tanzania juu ya namna wanavyopaswa kufanya kazi zao,iliyofanyika leo katika Hoteli ya New Afrika,jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wanahabari waliohudhulia Semina hiyo wakifatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa toka kwa baadhi ya wanahabari nguli barani Afrika walioongoza semina hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...