Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk.
Florens Turuka (wa pili kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa
REPOA, Prof. Samuel Wangwe (kulia) wakati wa mkutano wa Taasisi ya Maafisa
Wakuu Watendaji (CEOs Round Table) katika semina kuhusu umuhimu wa kutumia
utaratibu huo wa KAIZEN kuchochea maendeleo Jumanne jijini Dar es Salaam. Wa pili kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya
Biashara na Viwanda, Bw. Uledi Musa na Muwakilishi wa Shirika la Kimataifa la
Japan (JICA) Tanzania, Bw. Yasunori Onishi (kushoto).
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Florens Turuka (katikati) akifuatilia jambo
wakati wa mkutano wa Taasisi ya Maafisa Wakuu Watendaji (CEOs Round Table)
katika semina kuhusu umuhimu wa kutumia utaratibu huo wa KAIZEN kuchochea
maendeleo Jumanne jijini Dar es Salaam.
Kulia ni Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada na Katibu Mkuu, Wizara ya
Biashara na Viwanda, Bw. Uledi Musa.
Watanzania
wameshauriwa kujifunza na kuutumia mfumo wa KAIZEN ambao unalenga kuongeza tija katika utendaji kazi, kuleta
ufanisi wa uzalishaji na ubora ili kuchochea maendeleo nchini.
Wito
huo ulitolewa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Florence Turuka wakati
akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara tu baada ya
kufungua mkutano wa Taasisi ya Maafisa Wakuu Watendaji (CEOs Round Table) katika
semina kuhusu umuhimu wa kutumia utaratibu huo wa KAIZEN kuchochea maendeleo. “Utaratibu
huu unalenga kuleta mabadiliko ya kifikra na ujuzi sehemu za kazi na kuongeza
ubora wa huduma zinazotolewa na kampuni au taasisi zetu hapa nchini,”alisema Dk.
Turuka aliyemuwakilisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
KAIZEN
ni dhana iliyoanzia na kutumika nchini Japan na kuaminika kuleta mapinduzi
makubwa ya maendeleo katika nchi hiyo ikilenga kufikiwa kwa mapinduzi ya
viwanda. Kimsingi,
mfumo huo unalenga kuongeza thamani na uzalishaji kwa kuwawezesha wananchi
mbinu mbinu bora za kazi na usimamizi katika maeneo yao ya kazi. “Utaratibu
huu ni wa mabadiliko ya fikra kwa wafanyakazi na waajiri wao sehemu za kazi na kutumia
fursa hiyo kuwawezesha wafanyakazi kupata ujuzi zaidi na vitendea kazi bora
kutoa huduma bora,”alisema.
Dk.
Turuka alisema utaratibu huo haulengi tu sekta binafsi, bali pia sekta ya umma
ambayo inatakiwa kushirikiana na sekta hiyo ili kufikia malengo ya nchi. Balozi
wa Japani nchini, Bw. Masaki Okanda alisema utaratibu huo ni wa kubadili fikra
kwa kampuni au taasisi katika uendeshaji kwa nia ya kuleta tija na ubora wa uzalishaji. “Japani
imefanikiwa sana katika utendaji na ubora huduma kupitia utaratibu huu wa
KAIZEN na mnaweza kuutumia mpate mafanikio,” alisema.
Alisema
Tanzania ina rasilimali nyingi na kuna kampuni na taasisi nyingi lakini inatakiwa
kuimarisha utaratibu wa kujenga ujuzi kwa ajili ya kuongeza tija na ubora wa
huduma. Alisema
panahitajika kuwawezesha wafanyakazi sehemu za kazi na kuweza kuleta mabadiliko
ya uzalishaji bora na kuwa kichocho katika kuleta mabadiliko ya maendeleo.
Naye,
Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Japan (JICA) Tanzania, Bw. Yasunori Onishi
aliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara na Tanzania KAIZEN Unit katika
jitihada inazozifanya kwa kushirikiana na shirika lao katika kuimarisha swala
hilo. Alisema
utaratibu huo uliasisiwa Japan na kuwapatia mafanikio makubwa ambao unalenga zaidi ushirikishwaji wa watu wa
chini.
Mfumo
huo sasa unatumika kama njia ya kuleta mabadiliko na tayari mataifa mbalimbali duniani
wanautumia zikiwemo nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kama Ghana, Kenya na
Zambia. Mhandishi
wa Kampuni ya TAPCO, Shabbier Khataw ambae kampuni yake inatumia mfumo huo alisema
umewaletea mafanikio makubwa katika utendaji, uzalishaji na ubora wa huduma
wanazotoa.
Hadi
sasa kuna kampuni 32 Tanzania ambazo zinatumia mfumo huu kwa majaribio. “Utaratibu
huu ni muhimu kama tunataka kuendelea katika sekta ya viwanda...ni viwanda
pekee ndivyo vitalikwamua taifa hili,”alisema.
Mkutano
huo wa majadiliano uliandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara, Tanzania KAIZEN
Unit Kwa kushirikiana na Shirika la kimataifa la Japani la JICA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...