Mkurugenzi wa Mafunzo kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Otilia Gowelle (kushoto) akizungumza jambo kuhusu msaada wa vifaa na vitabu vya miongozo kwa ajili ya mafunzo ya matabibu wasaidizi kwenda kwenye ngazi ya Tabibu viliovyokabidhiwa kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa Kituo cha Kimataifa cha Mafunzo na Elimu( I-TECH TZ), Dkt Fatma Kabore(kulia) wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika leo jijini Dares Salaam kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo.
Mwakilishi Mkazi wa Kituo cha Kimataifa cha Mafunzo na Elimu( I-TECH TZ), Dkt Fatma Kabore(kushoto) akimkabidhi tablet kwa ajili ya mafunzo ya masafa ya matabibu wasaidizi kwenda kwenye ngazi ya Tabibu Mkurugenzi wa Mafunzo kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Otilia Gowelle wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika leo jijini Dares Salaam kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo. Kituo hicho kimekabidhi tablet 71 zenye thamani ya Sh. milioni 24 kati hizo 60 zitatumia na wanafunzi wa fani hizo kwenye vyuo vya Mtwara, Kilosa na Mafinga na nyingine zitatumiwa na wakufunzi.
Mwakilishi Mkazi wa Kituo cha Kimataifa cha Mafunzo na Elimu( I-TECH TZ), Dkt Fatma Kabore(wa pili kutoka kushoto) na Mkurugenzi wa Mafunzo kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Otilia Gowelle(wa nne kutoka kulia) wakiwa na watendaji wengine wa wizara hiyo na kutoka kituo hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Hongera DR Gowelle kwa uchapakazi uliotukuka ,pamoja na team yako yote

    ReplyDelete
  2. It is slightly reassuring to see even drs to be troubled with obesity, they are after all humans, predisposed to the sweet tooth and the urge to munch much and laden ourselves with lard!
    Unfortunately we don`t exercise as much as we should.
    Dear fellow Drs, cut the carbs and start the old good "TIZI".
    Dr Bitozi.

    ReplyDelete
  3. Huko kwenye maofisini hamna vijana, mbona kila siku ni wazee tu ndio wanenda kwenye haya mafunzo, warsha , makongamano, ni lini pia tutawajengea uwezo vijana wetu??

    Mdau wa maendeleo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...