Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Jumanne Sagini akionyesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) Daftari la Wapiga Kura linalotumika kuandikisha wananchi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Kushoto ni Mratibu wa Uchaguzi huo Bw. Denis Bandisa.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini akiongea na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Desemba 14 mwaka huu ambapo amesema hadi sasa maandalizi yote yamekamilika. Kushoto ni Mratibu wa Uchaguzi huo Bw. Denis Bandisa na kulia ni Afisa Mwandamizi wa TAMISEMI Bw. Mohamed Mavura.

 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini akitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye  Daftari la Wapiga Kura ili waweze kushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu. Pia Katibu Mkuu huyo amewataka Viongozi wote wanaosimamia uchaguzi huo kuzingatia sheria na kanuni za uchaguzi. Kushoto ni Mratibu wa Uchaguzi huo Bw. Denis Bandisa na kulia ni Afisa Mwandamizi wa TAMISEMI Bw. Mohamed Mavura.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini  akitoa wito kwa Viongozi wa Vyama vya Siasa, Wagombea na Washabiki wao kuendesha kampeni kwa amani, utulivu na ustaarabu bila kukiuka kanuni na taratibu zilizowekwa. Kushoto ni Mratibu wa Uchaguzi huo Bw. Denis Bandisa.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Jumanne Sagini akionyesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2014 ambazo tayari zimesambazwa kwa wadau wote wa uchaguzi huo. Aidha amesema kuwa Kanuni hizo zimewekwa katika Tovuti ya TAMISEMI ambayo ni www.ps@pmoralg.go.tz . Kushoto ni Mratibu wa Uchaguzi huo Bw. Denis Bandisa.



Mratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kutoka TAMISEMI Bw. Denis Bandisa akifafanua utaratibu wa kumuandikisha Mpiga Kura katika Daftari laWapiga Kura wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Amesema Serikali imetenga Shilingi Bilioni 20 kwa ajili ya Uchaguzi huo. (PICHA NA MAELEZO).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...