Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wa tatu kutoka (kushoto) Makamu wa Rais wa
Kenya, William Ruto, (kushoto kwake) Makamu wa Rais kwanza wa Burundi,
(kulia kwake) wakijumuika kwa pamoja na viongozi wengine wakionyesha
Taarifa ya pamoja waliyoisaini kuhusu majadiliano ya kuimarisha
Miundombinu kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,
katika mkutano wa 3 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) kuhusu
Miundombinu, uliofanyika kwenye Ukumbi wa KICC, jijini Nairobi jana
Novemba 29, 2014. Picha na OMR.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya viongozi wakati wakitoka
kwenye Ukumbi wa mikutano wa KICC, baada ya kushiriki katika mkutano wa
3 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) kuhusu Miundombinu
uliofanyika jijini Nairobu, Kenya jana Novemba 29, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na viongozi
wengine walioshiriki katika mkutano huo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, kifurahia jambo na Makamu wa Rais wa Kenya
William Ruto na Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, wakati
wakiondoka katika viwanja vya Ukumbi wa mikutano wa KICC, baada ya
kushiriki kwenye mkutano wa 3 wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC)
kuhusu Miundombinu, uliofanyika jijini Nairobi, Kenya jana Novemba 29,
2014. Picha na OMR.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...