Hii ndio Barua iliyoandikwa na Miss Tanzania 2014,Sitti Mtevu kwenda kwa kampuni ya Lino International Agency ambao ndio waandaaji wa mashindano hayo ya Urembo hapa nchini.

Aliyekuwa
Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu katika pozi na mshindi wa pili,
Lillian Kamazima (kulia) aliyechukua nafasi yake pamoja na mshindi wa
tatu, Jihhan Dimachk.
Sitti
Abas Mtemvu amelivua taji hilo baada ya kuiandikia barua Kamati ya Miss
Tanzania, November 5 mwaka huu, kuhusiana na uamuzi wake huo.
Mrembo
huyo alikuwa akikabiliwa na shutuma za kudanganya umri wake, jambo
ambalo lilililazimu Baraza la Sanaa la Taifa, (Basata) kutokana na agizo
la wizara husika kufuatilia ukweli wake.
“Baada ya kutwaa taji la urembo la Miss Tanzania kumezuka shutuma mbalimbali dhidi yangu. Wameniwekea maneno mengi sana mdomoni kwamba nimesema wakati siyo,” amesema kwenye barua hiyo.
“Baada ya kutwaa taji la urembo la Miss Tanzania kumezuka shutuma mbalimbali dhidi yangu. Wameniwekea maneno mengi sana mdomoni kwamba nimesema wakati siyo,” amesema kwenye barua hiyo.
Miss Tanzania aliyechukua nafasi ya Sitti Mtemvu, Lilian Kamazima pichani kulia.
“Shutuma
hizo zimeandikwa katika vyombo mbalimbali vya habari, blogs na mitandao
ya kijamii, kiasi ambacho naweza hata kuhatarisha maisha yangu. Sasa
kwa hiari yangu tena bila kushawishiwa na mtu na kwa kulinda heshima
yangu na familia yangu natamka rasmi kuvua taji la urembo la Miss
Tanzania 2014,” ameongeza.
“Napenda niwashukuru wale wote waliokuwa wakinipa sapoti tangu mwanzo nilipoingia katika mashindano haya katika ngazi ya taifa, na warembo wote wa Chang’ombe, Temeke pamoja na wote tuliokuwa nao katika fainali za Taifa. Pia napenda kutuma shukrani za dhati kwa waandaji wote wa kituo cha Chang’ombe, Temeke na wajumbe wa Kamati ya Miss Tanzania kwa mafunzo mbalimbali niliyopata. Nawashukuru pia waandishi wote kwa mchango wenu, pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo na Baraza la Sanaa kwa busara zenu.”
“Napenda niwashukuru wale wote waliokuwa wakinipa sapoti tangu mwanzo nilipoingia katika mashindano haya katika ngazi ya taifa, na warembo wote wa Chang’ombe, Temeke pamoja na wote tuliokuwa nao katika fainali za Taifa. Pia napenda kutuma shukrani za dhati kwa waandaji wote wa kituo cha Chang’ombe, Temeke na wajumbe wa Kamati ya Miss Tanzania kwa mafunzo mbalimbali niliyopata. Nawashukuru pia waandishi wote kwa mchango wenu, pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo na Baraza la Sanaa kwa busara zenu.”
Aliyekuwa Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu katika pozi.
“Leo
nalivuta taji rasmi nililopewa na binadamu lakini alilonipa mwenyezi
Mungu bado ninalo. Mwisho naomba radhi Watanzania wote kwa uamuzi huo
niliochukua.” Nafasi yake imechukuliwa na aliyekuwa mshindi wa pili,
Lilian Kamazima.
Sour looser. Not even a word of congratulation to her successor!
ReplyDeleteBado hajutii kudanganya kwake. Anaona watu tu wamemsakama bila sababu. Wabongo iko kazi kweli kweli.
ReplyDeleteHuyu wa sasa ndio ana umri gani? mi naona kama wale wale tu.
ReplyDeleteHata kama kalivua hilo taji bado tunataka kujua kauli ya uchunguzi toka baraza la michezo na kama ni kweli alidanganya na arudishe taji la changombe-Temeke
ReplyDeleteTehtehteh bado unamalizia na jeuri yenye kiburi dah rekebisha moyo wako hata kumpongeza mwenzako unaona watu wamekufanyia Choyo? Choyo umejifanyia mwenyewe na kuhusu kuvaliwa na watu na mungu amekupa bado unalo ni kweli ila kumbuka Mungu umeongopea wanadamu wake pia kwahiyo tubia kwa mungu na wacha tabia yako chafu ya roho.
ReplyDeleteMazoea ya kuhalalisha haramu kuwa halali
ReplyDeleteWatanzania tubadilike...huyu binti yafaa awajibishwe kwa yote yaliyotokea. Huu pia ni aina ya UFISADI!!! Taasisi zilizohusika ikiwa ni pamoja na RITA na kamati ya mashindano ya bwana Lundenga pia nao wawajibike na ikishindikana basi wawajibishwe.
ReplyDeleteBwana Lundenga wewe ni mwana Yanga mwenzangu, lkn kwa huu upuuzi unaofanya ktk tasinia hii ya urembo sitakuwa nawe. Inawezekanaje moja ya vielelezi muhimu (cheti cha kuzaliwa) ktk mashindano kipatikane siku chache
ReplyDeletekabla ya kufanyika?????? Vielelezi hivi yafaa viwasilishwe mapema pindi mashindano yanapoanza siyo kama alivyofanya huyo mrembo wako!
Vipi sasa kuhusu kuwa mcha Mungu? Kwani umekiri kuna taji kakupa! Ili iwe shukurani kutoka kwako.
ReplyDeleteNilikuwa sifuatilii mjadala ila huyo namba mbili moto...
ReplyDeleteInabidi arudishe zawadi alizopewa na taji la mis temeke na chang'ombe
ReplyDeleteAibu hii isiishie kwa Sitti pekee, Lundenga na hao majaji walio husika kumpitisha inatakiwa wawajibike. Ikiwezekana mashindano yasiratibiwe na Lundenga tena, bali iwepo taasisi rasmi inayotambulika na serikali. Reeds wajiangalie mara mbili, kufadhili vitu vivyoo jaa ujanja na upotoshaji kwenye jamii.
ReplyDelete