Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(Kazi Maalum) Profesa Mark Mwandosya leo amemaliza ziara yake ya siku sita nchini Ethiopia kwa kukagua ujenzi wa Ofisi za Bonde la Mto Abay (White Nile),kutembelea chanzo cha Mto Abay,na kutembelea maporomoko maarufu ya Mto Abay (White Nile).
Waziri Mwandosya,kushoto,akiwa na Mhaidrolijia Mengistu,Mkurugenzi Mkuu wa Bone la Mto Abay baada ya kukagua kazi zinazoendelea za ujenzi wa Makao Makuu ya Bonde mjini Bahar Dar, Amhara.
Waziri Mwandosya kwenye mti uliopandwa na mwakilishi wa Tanzania wakati wa kuweka jiwe la msingi wa Jengo wakati wa sherehe za Siku ya Nile, mwaka 2013.
Waziri Mwandosya,kushoto,na Mhaidrolojia Mengistu, kulia,na Mama Lucy Mwandosya,katikati,wakiwa kwenye maporomoko ya Mto Abay,yaliyo 'Kebele'ya Tis Abay.
Waziri Mwandosya na Mama Lucy Mwandosya wakiwa na wenyeji wao wa Gish Abay, Wilaya ya Sekela,chanzo cha Mto Blue Nile, kilicho kilomita 150 kutoka Bahar Dar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tunaomba wahusika Mh Mwandosya awe Rais 2015.

    Mungu tunaomba pokea maombi yetu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...