Na Mwandishi Maalum, New York
Shirika la Umoja wa Mataifa
linalohudumia wakimbizi ( UNHCR) linakabiliwa na upungufu mkubwa wa
raslimali fedha kiasi cha kuathiri utoaji wa misaada ya kibinadamu kwa wakimbizi wanaoendelea kuongezeka kila mwaka.
Hayo yameelewa siku ya
jumatano na Kamishna Mkuu wa UNHCR, Bw. Antonio Guterres
wakati alipokuwa akiwasilisha taarifa
ya Shirika hilo mbele ya wajumbe wa Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu
la Umoja wa Mataifa.
Katika taarifa yake
hiyo ambayo imeainisha utejaji wa UNHCR
katika kipindi cha mwaka uliopita, mafanikio na changamoto , Bw. Guterres amesema, idadi ya wakimbizi kwa
mwaka 2013 ilikuwa zaidi ya watu milioni 50 ikiwa ni idadi kubwa tangu Vita Kuu
ya Pili ya Dunia. Na kwamba idadi hiyo inaweza kuongezeka ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.
Amesema, idadi ya wakimbizi wa ndani katika Afrika imeongezeka kutoka wakimbizi milioni 10.4 na kufikia milioni 12.5.
Aidha ameongeza kuwa wanawake na watoto chini ya miaka 18 ndio kundi kubwa zaidi .
Kundi ambalo amesema linakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwamo za udhalilishwaji wa kijinsia, ndoa za utotoni, biashara ya haramu ya binadamu ambapo wengi
wao huuzwa na kugeuzwa watumwa.
Amesema ongezeko hilo
la wakimbizi haliendani na raslimali
fedha na misaada mingine hali inayolifanya kutowafikia wakimbizi wengi kwa wakati na pia Shirika kulazimika kupunguza hata kipimo cha chakula ambacho
wakimbizi wanapewa hususani Barani
Afrika.
Amebainisha kuwa
Afrika inahitaji msaada wa haraka wa dola 186 milioni ili wakimbizi waweze kupata mlo
kamili kwa mwaka huu wa 2014. Aidha Kupunguzwa
kwa kipimo cha chakula kumesababisha
watoto wengi kupata utapia mlo.
Amezitaja baadhi ya sababu zinazopelekea uzalishaji mkubwa wa
wakimbizi kuwa ni vita vya wenyewe kwa wenye, ukame , uhaba wa maji na mabadiliko ya tabia nchi.
Aidha ameeleza kuwa
kwa upande wa Bara la Afrika ambalo limeshuhudia ongezeko la wakimbizi kumetokana na vita vya wenyewe kwa wenye katika nchi za
Mali, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sudani
ya Kusini, Somalia na baadhi ya maeneo
ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Eneo jingine ambalo Kamishna amelitaja kuzalisha wakimbizi
wengi ni pamoja na Mashariki ya Kati hususani Syria.
Kamishna Mkuu pamoja
na kuhimiza Jumuiya ya Kimataifa
kuendelea kulichangia Shirikia hilo ili
liweze kuendelea na jukumu la utoaji wa
misaada ya kibinadamu. Amesisitiza kuwa suluhisho pekee la kumaliza tatizo la kuwapo kwa wakimbizi ni la
kisiasa zaidi kwa pande zinazohusika
kumaliza tofauti zao.
Amesema, wanasiasa hawawezi kuendelea kuwa chanzo cha
migogoro na machafuko yanayopelekea wananchi wao kuyakimbia makazi yao na nchi zao na kisha kuyaachia Mashirika yanayotoa misaada ya kibinadamu jukumu la
kuwahudumia wahanga wa machafuko hayo.
“ Tufikie mahali sasa tubadilike na tulikatae hili, haiwezekani wengine
waazishe machafuko na kuwaachia watu wengine wasafishe uchafu wao”
amesema Bw.
Aidha ametumia mkutano huo kuzishukuru nchi mbalimbali
ambazo kwa muda mrefu zimekuwa wenyeji
wa wakimbizi ikiwa ni pamoja na kutumia raslimali zao kuwasaidia.
Akasema nchi hizo
ikiwamo Tanzania zimeratibu na kuwezesha
baadhi ya wakimbizi kurejea makwao kwa hiari ikiwani ni
pamoja na kuwapatia uraia kwa
wale ambao wameomba.
Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania, Balozi Ramadhan
Mwinyi, akizungumza kwa niaba ya
SADC amesema Jumuiya hiyo
inapinga kuendelea kuitegemea UNHCR hata katika mambo ambayo nchi mwenyeji inaweza
kuyatekeleza.
Akatoa mfano wa baadhi ya majukumu ambayo nchi mwenyeji
inaweza kuyatekeleza pasipo kutegemea UNHCR
kuwa ni pamoja na ukusanyaji wa
takwimu na utambuzi wa wakimbizi.
Amesema jukumu ambalo
UNHCR inaweza kuchangia ni katika uwezeshaji na si utekelezaji wa zoezi
lenyewe kutokana uenyeti wake.
Kuhusu kupungua kwa
bajeti ya Shirika hilo, SADC imeelezea wasi wasi wake kuwa pamoja na athari ambazo zimeanza kujitokeza
pia kutaathiri uwezo wa nchi wenyeji kuendelea kutoka huduma kwa wakimbizi na hasa
ikizingatiwa kuwa pamoja na matatizo ya kiuchumi waliyonayo bado nchi hizo zimekuwa zikitumia raslimali zake
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...