UZINDUZI wa filamu ya Wape Salamu Zao unatarajia kufanyika siku ya Jumapili tarehe 9 November katika ukumbi Travetine Magomeni, jijini Dar es salaam.
Uzinduzi huo utambatana na ujio wa sesson 2 kipindi cha Ulimwenguni wa filamu cha TBC 1,kinachoongozwa na Juma Mtetwa katika, kivutio kikubwa ni Jackson Kabirigi ‘Kisate’.
“Nimepanga kuacha historia katika uzinduzi wa filamu ya Wape Salamu Zao, kuna vitu vingi sana ambavyo sijawahi kuwaonyesha watazamaji hajawahi kuviona kutoka kwangu tarajieni maajabu,”anasema Kabirigi.
Uzinduzi huu unasindikizwa na gwiji la muziki wa Taarab Bongo mfalme Mzee Yusuf, ambaye naye ameahidi kufanya show ya kipekee haijawahi kutokea hivi karibuni, na kuimba nyimbo zinazotamba na kufanya vizuri Tanzania.
Wasanii nyota wa filamu kutoka Bongo movie watakuwepo wakiwa wamependeza huku zuria jekundu likipamba sehemu ambayo watu watapata nafasi ya kupiga piga katika mapozi, show hiyo ya kufunga mwaka kiingilio ni 8,000/ tu kwa mtu mmoja si ya kukosa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...