Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) na Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima wakifuatilia kongamano la uwekezaji lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) na kuhusisha wawekezaji mbalimbali kutoka nje ya nchi. Kongamano hilo lililolenga kuvutia uwekezaji katika miradi ya BRN lilifanya jijini Dar es Salaam Jumatano. Kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu akifafanua kuhusu fursa mbalimbali za uwezekaji zilizopo katika shirika hili wakati wa kongamano la uwekezaji la BRN.
Baadhi ya washiriki waliohudhuria kongamano la uwekezaji la BRN. Kongamano hilo lililoandaliwa na Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji na Usimamizi wa Miradi (PDB) ambayo ndiyo inayosimamia mpango wa BRN lilivutia wawekezaji mbalimbali kutoka nje ya nchi. (Picha na Idara ya Mawasiliano PDB)
Mkurugenzi wa Masoko wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),David Shambwe akimueleza jambo  mmoja wa washiriki wa kongamano la wawekezaji la BRN juu ya miradi mbalimbali iliyopo sasa katika shirika la nyumba.
Afasa Masoko kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),Mariam Ndabagenda akimuonesha mmoja wa washiriki wa kongamano la wawekezaji la BRN juu ya miradi mbalimbali iliyopo sasa katika shirika la nyumba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...