Makamu
wa Rais wa Mfuko wa Changamoto za Millenia (MCC) Kamran Khan ( wa
kwanza kushoto ) akimweleza jambo Waziri wa Nishati na Madini Profesa
Sospeter Muhongo (wa kwanza kulia) anayesikiliza katikati ni Balozi wa
Marekani nchini, Mark Childress mara baada ya kikao hicho.

……………………………………………………………………
Na Asteria Muhozya, Dar es Salaam
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Makamu wa Rais wa Mfuko wa Changamoto za Millenia (MCC) Kamran Khan na Ujumbe wake akiwemo Balozi wa Marekani nchini Mark Childress, katika kikao kilicholenga kujadili maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa MCC Awamu ya pili na masuala ya kuendeleza sekta ya nishati nchini.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Makamu wa Rais wa Mfuko wa Changamoto za Millenia (MCC) Kamran Khan na Ujumbe wake akiwemo Balozi wa Marekani nchini Mark Childress, katika kikao kilicholenga kujadili maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa MCC Awamu ya pili na masuala ya kuendeleza sekta ya nishati nchini.
Kikao
hicho kimezihusisha pia taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na
Madini ikiwemo, Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Shirika la Umeme
Tanzania (Tanesco), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Shirika la
Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Kampuni ya Uendelezaji Jotoardhi
Tanzania (TGDC) pamoja na taasisi nyingine za Serikali ikiwemo Shirika
la Maendeleo la Taifa (NDC) na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na
Nishati (EWURA).
Katika
kikao hicho, Profesa Sospeter Muhongo amezitaka taasisi hizo kutekeleza
miradi hiyo kwa kasi zikizingatia suala la uwajibikaji, ubunifu, uwazi
na kuongeza kuwa, miradi hiyo itatekelezwa bila kuwepo na mazingira ya
rushwa , huku akisisitiza ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi
katika uendelezaji wa miradi hiyo.
Kwa upande wake Makamu wa Rais wa MCC, Kamran Khan ameahidi kutoa ushirikiano kwa Wizara katika kutekeleza miradi hiyo ambayo inalenga kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa na umeme wa uhakika na wa kutosha.
Kwa upande wake Balozi wa Marekani nchini Mark Childress amesisitiza suala la kuzingatia muda katika utekelezaji wa miradi hiyo na kuongeza kuwa, hakuna sababu itakayokwamisha miradi hiyo.
Kwa upande wake Makamu wa Rais wa MCC, Kamran Khan ameahidi kutoa ushirikiano kwa Wizara katika kutekeleza miradi hiyo ambayo inalenga kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa na umeme wa uhakika na wa kutosha.
Kwa upande wake Balozi wa Marekani nchini Mark Childress amesisitiza suala la kuzingatia muda katika utekelezaji wa miradi hiyo na kuongeza kuwa, hakuna sababu itakayokwamisha miradi hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...