Kaimu Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Jimmy Myalize (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo akitoa ufafanuzi wa tatizo la huduma za kibenki kupitia mtandao wa simu za mkononi (Mobile Banking) ambapo alisema licha ya tatizo hilo hakuna hata senti moja ya mteja wao iliyopotea. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Masoko na Mawasiliano, Rukia Mtingwa.
 Kaimu Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Rukia Mtingwa (kulia) akitoa ufafanuzi kuhusu tatizo lililojitokeza jana katika huduma zao za kibenki kupitia mtandao wa simu za mkononi (Mobile Banking) ambapo alisema licha ya wateja kutoona salio katika akaunti zao hakuna hata senti moja iliyopotea. Kushoto ni Kaimu Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa NBC, Jimmy Myalize.
Baadhi ya wanahabari wakiwa kazini kurekodi mkutano wa menejimenti ya Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) jijini Dar es Salaam leo walipokuwa wakitoa ufafanuzi juu ya tatizo lililojitokeza jana Desemba 3, 2014 ambapo wateja wa benki hiyo walishindwa kutumia huduma za kibenki kupitia mtandao wa simu za mkononi (Mobile Banking).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...