KIKOSI cha timu ya Friends Rangers (pichani), kesho kinajitupa
kwenye Uwanja wa Makurumla, Magomeni Mwembechai, Dar es salaam kuvaana na timu ya Ndanda FC ya Mtwara katika mchezo
wa kirafiki wa kijiandaa na mzunguko wa pili wa ligi daraja
la kwanza.
Ofisa habari wa timu hiyo Asha Kigundula, alisema kikosi
hicho kinashuka dimbani kikiwa ni sehemu ya maandalizi ya
mzunguko wa pili wa ligi hiyo inayoanza kutimua vumbi
Ijumaa ya Desemba 26, 2014.
Alisema kwa kutambua umuhimu wa michuano hiyo ambapo
wao wataanzia ugenini dhidi ya Lipuli ya Iringa, imejipanga
kupata mechi kadhaa za kirafiki, ambapo kesho Jumapili
itakuwa na mchezo mwingine dhidi ya Ruvu Shooting.
Kigundula alisema kuwa kikosi chao kipo katika maandalizi
makali ya kuhakikisha kinaendeleza rekodi yake ya
kutofungwa kama ilivyokuwa katika mzunguko wa kwanza
wa michuano hiyo.
Alisema timu yao chini ya kocha wake Ally Yusuph 'Tigana'
kimewasajili Haruna Moshi 'Boban' Amir Maftah, na Robert. Wengine ambao wamekuja kwa mkopo Wine Abbas kutoka
Ruvu Shooting na Mahmoud Osman kutoka Coastal Union.
"Tunaendelea kukinoa kikosi chetu kwa kupata mechi nyingi
za kirafiki lengo letu ni kuendelea na safari yetu ya kupanda
daraja, ambapo msimu ujao tunataka kucheza ligi kuu"alisema
Kigundula.
Friends Rangers inashika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi
daraja la kwanza, huku Majimaji ikishika usukani wa ligi hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...