Hivi karibuni Idara ya uhamiaji mkoa wa Njombe iliunga mkono jitihada za mkuu wa wilaya ya makete Josephine Matiro kusaidia vituo vya watoto yatima wilayani humo kwa kutoa msaada wa zaidi ya shilingi milioni 1

Akizungumza wakati akikabidhi msaada wao afisa uhamiaji mkoa wa Njombe Rose Mhagama alisema wameguswa na suala hilo na kuamua kuvisaidia vituo vya watoto yatima Makete vitu mbalimbali, na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kuwasaidia watoto hao

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya Hiyo Bi Josephine matiro amewataka wanamakete kubadilika na kuacha dhana kuwa watoto hao watasaidiwa na wafadhili kutoka nje na badala yake nao wawasaidie watoto hao kwa kitu chochote walichojaliwa na Mungu

Vituo vilivyonufaika ni Nyumba ya yatima Bulongwa, Fema Matamba na Kituo kipya cha Kisinga
 Watoto yatima wakipewa zawadi na Idara ya uhamiaji mkoa wa Njombe
Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akiwa amembeba mtoto yatima anayelelewa kituo cha Nyumba ya yatima Bulongwa
 
 Baadhi ya msaada uliotolewa
 Mkuu wa wilaya akikabidhiwa msaada huo na afisa uhamiaji mkoa wa Njombe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...