Na Bashir Yakub
Katika adhima ya ya mwendelezo wa makala za namna ya kuendesha kampuni leo tena tuangalie kuhusu hisa na hasa namna ya kuhamisha hisa.
HISA NININI.
Kwa maana ambayo inaweza kueleweka kwa wepesi zaidi ni kusema kuwa hisa ni aina ya maslahi ya mtu ya katika kampuni.Natumia neno aina kwakuwa maslahi katika kampuni ni mengi si hisa tu isipokuwa hisa ni mojawapo ya maslahi. Hivyo kile ambacho mtu anamiliki katika kampuni ndio hisa zake. Hisa hutofautiana kutokana na uwezo wa mtu kwa maana wapo wenye hisa ndogo wapo wenye kubwa na kati.
KUUZA NA KUNUNUA HISA.
Hisa ni mali inayohamishika. Ni mali sawa na mali nyingine zozote zinazohamishika. Kama ambavyo mali nyingine zinaweza kununuliwa au kuuzwa, kutolewa zawadi na kurithiwa ndivyo pia hata hisa zinavyoweza kuwa.Hii yote huitwa kuhama kwa hisa. Kuhama kwa hisa kwa lugha ya kitaalam ambayo ndio hutumika katika katiba za makampuni ni ( Transfer of shares). Mara nyingi suala la kuuziana hisa linawahusu wanahisa wenyewe na hivyo wanahisa wanapokuwa wameuziana hisa au wamepeana zawadi ni lazima nyaraka inayoonesha muamala huo wa mauziano au zawadi ambayo ina muhuli wa wakili iwasilishwe kwenye uongozi wa kampuni kwa ajili ya kusajiliwa. Kama hakuna nyaraka yoyote iliyowasilishwa mbele ya kampuni kuthibitisha uhamisho ni kosa kampuni kusajili uhamisho au mauziano hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...