Na Anna Nkinda – Lindi

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amewataka wakazi wa Kata ya Ng’apa wilaya ya Lindi mjini kuchagua viongozi waadilifu na wenye sifa ambao watawaongoza wananchi kusimamia shughuli za maendeleo yao.

Mama Kikwete ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia wilaya ya Lindi mjini alitoa rai hiyo jana wakati akiongea na wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni ya uchaguzi wa Wenyeviti na Wajumbe wa Serikali za mitaa uliofanyika katika Kata hiyo.

Mama Kikwete alisema kuna baadhi ya watu wanachagua viongozi kwa ushabiki pasipo kuangalia kiongozi huyo kama ana sifa au la, na kuwasisitiza wananchi hao  siku ya uchaguzi ikifika wasifuate mambo ya ushabiki na kuchagua kiongozi kwani ushabiki hauna manufaa yoyote.

“Nawaombeni muwapigie kura za ndiyo viongozi wote wa  CCM wanaogombea nafasi za Wenyeviti na Wajumbe wa Serikali za Mitaa,  kwani hawa wanasifa na mkiwachagua kutakuwa  na manufaa kwenu na vizazi vyenu hivyo basi wote mliojiandikisha  siku ya uchaguzi ikifika mjitokeze  kupiga kura na kukichagua  Chama chetu”, alisema .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tanzania inahitaj viongozi walio na hari ya kuleta maendeleo na kushirikisha wananchi wote katika kuendeleza nchi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...