Na Anna Nkinda – Lindi
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amewataka wakazi wa Kata ya Ng’apa wilaya ya Lindi mjini kuchagua viongozi waadilifu na wenye sifa ambao watawaongoza wananchi kusimamia shughuli za maendeleo yao.
Mama Kikwete ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia wilaya ya Lindi mjini alitoa rai hiyo jana wakati akiongea na wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni ya uchaguzi wa Wenyeviti na Wajumbe wa Serikali za mitaa uliofanyika katika Kata hiyo.
Mama Kikwete alisema kuna baadhi ya watu wanachagua viongozi kwa ushabiki pasipo kuangalia kiongozi huyo kama ana sifa au la, na kuwasisitiza wananchi hao siku ya uchaguzi ikifika wasifuate mambo ya ushabiki na kuchagua kiongozi kwani ushabiki hauna manufaa yoyote.
“Nawaombeni muwapigie kura za ndiyo viongozi wote wa CCM wanaogombea nafasi za Wenyeviti na Wajumbe wa Serikali za Mitaa, kwani hawa wanasifa na mkiwachagua kutakuwa na manufaa kwenu na vizazi vyenu hivyo basi wote mliojiandikisha siku ya uchaguzi ikifika mjitokeze kupiga kura na kukichagua Chama chetu”, alisema .
Tanzania inahitaj viongozi walio na hari ya kuleta maendeleo na kushirikisha wananchi wote katika kuendeleza nchi.
ReplyDelete