Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amelaumu watu fulani ndani ya chama tawala cha ZANU-PF kwamba wanapanga kumng'atua mamlakani.

Akihutubia kongamano la chama hicho, Mugabe amesema kuwa kuna majaribio ya kuwahonga wajumbe kumpinga kama kiongozi, lakini wajumbe hawawezi kupokea hongo.


Kwa hilo amesema kuwa atapambana na rushwa ndani ya chama na kukabiliana na maafisa wa chama ambao kazi yao ni kutoa hongo.Wanachama wengi wa chama hicho wangali ni wafuasi sugu wa Rais Mugabe


Hasira ya Mugabe iliokana na madai ya njama ya kumuua yaliyotolewa dhidi ya naibu wake Joyce Mujuru. Hata hivyo Mujuru alikanusha madai hayo ambayo yamekuwa yakimuandamana.

Mugabe alisema kutokuwepo kwa Bi Mujuru kwenye mkutano huo wa chama kunaonyesha kuwa anaogopa.


Kadhalika Mugabe amesema Mujuru ni mwizi anayepanga kumuondoa mamlakani kwa kushirikiana na maafisa wengine wa chama.Maelfu ya wajumbe wa chama walihudhuria kongamano hilo mjini Harare


Chama tawala cha Zimbabwe kinakumbwa na vita vya ndani kwa ndani kuhusu ni nani atakayerithi nafasi ya Mugabe ambaye ana miaka 91 na ameilongoza taifa hilo tangu lijinyakulie uhuru.

Vilveile kiongozi huyo ametupilia mbali dhana ya kujiuzulu akisema ni upuzi .


Hivi karibuni afisa mwingine mkuu wa chama tawala, Robert Gumbo aliambia BBC kwamba Mugabe amwenye umri wa miaka 90 amegeuza chama tawala na kukifanya mali yake binafsi.
Bi Joyce Mujuru amedaiwa kupanga njama ya kumuua Mugabe ili achukue mamlaka kutokla kwake.


Bwana Gumbo alisema kuwa lengo kuu la Mugabe ilikuwa kuendeleza uongozi wa chama kwa niaba ya mke wake Grace.

Bi Mujuru ambaye amekanusha madai hayo alionekana kama mtu ambaye anegchukua uskani wa chama kutoka kwa Mugabe ambaye walipigania naye uhuru wa nchi hio kutoka mikononi mwa watwala wazungu. 

CHANZO: BBC SWAHILI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Ningekutana na Mugabe ningemwambia amuachie mama Joyce yeye abaki kiongozi wa chama

    ReplyDelete
  2. Uzushi wa viongozi wengi wa Afrika ni kung'ang'ania madarka na hakuna mapinduzi wanayofanya zaidi ya kuwaletea umaskini watu na wao kunufaika zaidi. Miaka 91 bado sing'atuki ng'o in maana gani" huo ni ulafi wa madaraka. Badilikeni

    ReplyDelete
  3. Mugabe na marehemu banda wa Malawi hawana tofauti anataka afie madarakani wamuache tu kwa sasa kwanza hatawali kutwa analala tu baba wa watu.

    mdau.
    mozambique

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...