Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Ofisi ya Hali ya Hewa ya Uingereza (UK Met Office) wamesaini mkataba wa makubaliano ya uboreshaji huduma za hali ya hewa hapa nchini. Mkataba huo umesainiwa tarehe 11 Novemba, 2014 wakati wa kikao cha masuala ya hali ya hewa (IBCS) kilichofanyika mjini Geneva Uswiss.

Akizungumzia makubaliano hayo Dkt Agnes Kijazi alisema Mamlaka ya Hali ya Hewa ililiomba Shirika la Hali ya Hewa Duniani kuisaidia TMA kuboresha huduma zake ili ziwe za kisasa (Modernization of meteorological services in Tanzania) na ofisi ya hali ya hewa ya Uingereza ilikubali kuisaidia TMA katika zoezi hilo. ‘Makubaliano tunayosaini leo ni sehemu tu ya kazi kubwa ya uboreshaji wa huduma za hali ya hewa nchini ambapo shirika la Kimataifa la Uingereza (DFID) kupitia Ofisi ya Hali ya Hewa ya Uingereza limeipatia TMA Pound 70,000’ alisema Dkt. Kijazi .

Akifafanua kuhusu matumizi ya fedha hizo Dkt. Kijazi alisema fedha hizo zitatumika kuijengea uwezo TMA kutunza data za hali ya hewa za kihistoria kwa njia ya digitali na pia kuwajengea uwezo watumishi wa TMA kutoa huduma bora zinazokidhi matarajio ya wadau na hivyo kulinda maisha ya watu na mali zao.

Kwa upande wake mkuu wa Ofisi ya Hali ya Hewa ya Uingereza Dkt. Rob Varley alisema anafurahia ushirikiano uliopo kati ya TMA na UK met office na akaahidi kuendeleza ushirikiano huo na pia kuisadia TMA kuboresha huduma zake.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa, Dkt. Agnes Kijazi akisaini mkataba na mtendaji mkuu wa Ofisi ya Hali ya Hewa ya Uingereza Dkt. Rob Varley. Tukio hilo lilishuhudiwa na Dkt. Ladislaus Chang’a, Mkurugenzi wa Utafiti katika Mamlaka ya Hali ya Hewa na Bi. Jane Wardle mtaalam wa masuala ya hali ya hewa kutoka ofisi ya hali ya hewa ya Uingereza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...