KOCHA wa Yanga Hans Van Puljim (pichani chini kulia) amedai kusikikitshwa na mlinda mlango Juma Kaseja (juu kushoto) kuingia kwenye bifu na uongozi wa klabu hiyo wakati alimtegemea kuongoza wachezaji wenzake siku za nyuma akiinoa timu hiyo.



Puljim ambaye alichukua nafasi ya Ernie Brandts mwaka jana kabla ya  kutimuliwa mara baada ya mechi ya Mtani Jembe mwaka jana ambapo Yanga ilinyukwa mabao 3-1 alimtumia Kaseja kuwa nahodha katika kikosi chake lakini leo amesema anasikia uchungu kumkosa mlinda mlango huyo.



"Nimefika hapa, hayupo Juma, hayupo Didier Kavumbagu, hayupo Hamisi Kiiza, kibinadamu kama watu ulizoea kufanya nao kazi ukasikia uongozi umewasaspendi, sitaki kujua sababu, wala sitaki kuingia masuala yao, lakini roho inaniuma, ni kama mwanafamilia akifariki, mtalia sana, roho zitauma, mtasikitika lakini mwisho wa siku maisha ni lazima yaendelee, "alisema Puljim ambaye unaweza kumwita "Kocha wa Mtani Jembe" kwani amechukua nafasi ya Mbrazil Marcio Maximo ambaye pia  amefungashiwa virago baada ya Yanga kuchukua kichapo cha mabao 2-0 katika mechi ya Mtani Jembe iliyofanyika Desemba 13 kwenye uwanja wa Taifa.
Kavumbagu
Puljim alisema "Nawaheshimu wachezaji waliopo, nimeshaongea nao jana (Jumamosi) ikiwa ni mazoezi yangu ya  kwanza kufanya nao. Kikubwa nimewambia wasahau yaliyopita, wasisikitike kuondoka kwa wenzao wasisikitike kuondoka kwa kocha. Yaliyopita yamepita sasa tuanze maisha mapya, tukiwa na lengo moja la kuifanya Yanga iwe juu.

"Kikubwa nilichowataka ni kujitambua, Yanga ni klabu kubwa. Kama mchezaji anapata nafasi basi lazima ajue jukumu lake. Mkakati wangu ni kuhakikisha Yanga inacheza soka la kuvutia na mpangilio mzuri. Najua wote ni binadamu na kuna makosa ya kibinadamu hutokea lakini ninawataka kila mmoja acheze kiushindani na morali ya hali ya juu.

"Kazi yangu kama kocha ni kuwajengea wachezaji morali, naipenda timu yangu, tunatakiwa tushirikiane viongozi watimize wajibu wao, mimi kama kocha nitimieze wajibu wangu, na wachezaji pia watimize wajibu wao wacheze kwa kutumia akili na soka la kuvutia.
Kiiza
Hata hivyo, Pluljim aligoma kuweka wazi fomesheni atakayotumia kuhakikisha Yanga inachukua taji la Ligi Kuu msimu huu kwa kile alichodai kuwa fomesheni sio inayofanya kushinda mchezo.
"Ushirikiano na kujituma ndio kunakowezesha kushinda mchezo, sina hofu na wachezaji, nina hofu na mbinu zangu nitakazowapa kama watazielewa na kuzitekeleza, kuna wachezaji wapya ambao siwafahamu miezi minne ya michache kusema naweza kuiweka Yanga kwenye kiwango cha juu, litawezekana kukiwa na ushirikiano wa kutosha."alisema
Puljim amesaini mkataba wa mwaka mmoja na nusu wa kuionoa timu hiyo hata hivyo amedai kuwa Yanga ni nyumbani itakapotokea ametimuliwa kabla ya muda wake kumalizika basi ataheshimu maamuzi ya uongozi ingawa hategemei hilo kutokea, kwa kuwa yeye ni mwanachama wa Yanga na amerudi nyumbani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...