Mkandarasi wa soko kuu la Mwanjelwa linaloendelea kujengwa jijini mbeya ndugu,Balwinder Singh kutoka katika kampuni ya (NECCO) amezungumza na Ripota wetu juu ya maendeleo ya soko hilo kubwa lenye zaidi ya maduka 400 ya biashara ndogondogo,Benki mbili na kituo kikubwa cha polisi ambapo amesema soko hilo anatarajia kulikabidhii mwakani (2015) mwezi wa tano.

Akiendelea kuzumza,Mkandarasi huyo amesema kuwa hali ya Ujenzi inaendelea vyema na wapo kwenye hatua za mwisho,hivyo hadi mwezi Mei mwakani soko litakuwa limekamirika kabisa na kulikabidhi.
Mkandarasi wa Ujenzi wa Soko kuu la Mwanjelwa jijini Mbeya,Balwinder Singh akiandika baadhi ya maelezo ya vipimo muhimu vya Ujenzi kama alivyokutwa na Kameramani wetu.
 muonekano wa mbele wa soko la Mwanjelwa. 
 muonekano wa nyuma wa soko hilo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongera sana Jiji la Mbeya! Maendeleo kama hayo ni hatua muhimu katika kukua kwa uchumi wa Jiji na wananchi kwa ujumla. Soko linaonyesha lina hadhi ya kimataifa, hivyo mjitahidi kufanya biashara kitaalam zaidi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...