KLABU ya Simba imeingia kambini leo Zanzibar huku ikimtema mshambuliaji wake raia wa Gambia Omar Mboob.
Katibu
mkuu wa Simba Steven Ally alidhibitisha kuwa mchezaji huyo ameenguliwa
kwenye kikosi cha Simba kwa vile ameshindwa kuonyesha kiwango cha
kumshawishi kocha Patrick Phiri ili aweze kusajiliwa.
"Mboob kwa
sasa tunamfanyia taratibu ili aweze kurudi nchini kwao, kesho (leo) au
kesho kutwa ataondoka, ameshindwa kuonyesha makali."alisema
Wakati
Ally akisema hayo, Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba Zakaria
Hanspope alisema "Mimi nilikutana na meneja wake katika shughuli zangu
za kibiashara akaniambia kijana wake ni mzuri na muda wowote atakwenda
kufanya majaribio barani Ulaya. Nikaona si mbaya akaja hapa
tukamwangalia, lakini kiwango chake bado” alisema Hanspope.
Hata
hivyo, tayari Simba imefikisha idadi ya wachezaji watano wa kigeni kwa
mujibu wa kanuni za Ligi ambao ni Dan Sserunkuma aliyechukua nafasi ya
Raphael Kiongera, Mganda Emmanuel Okwi, Joseph Owino na warundi Pierre
Kwizera na Amissi Tambwe.
Katika hatua nyingine, Simba imeingia
kambini Zanzibar jana jioni kujiandaa na mechi yao dhidi ya Yanga huku
makocha wa timu hizo kila mmoja ana matumaini ya kushinda mchezo huo
huku kocha wa Yanga Marcio Maximo akiingia mchecheto na kutamka kuwa
"Kocha anaajiriwa ili afukuzwe, hayo ndio maisha hasa Afrika, sihofii
kufukuzwa iwapo tutafungwa na Simba, ninachoangalia si tu mechi ya mtani
Jembe bali na za ligi.
Kauli ya Maximo aliiotoa baada ya
kuulizwa, kocha Ernie Brandts alitimuliwa baada ya matokeo ya mechi ya
mtani jembe msimu uliopita, na yeye amejiandaje katika hilo.
"Kocha
anaajiriwa ili afukuzwe, mimi sijali, matokeo yoyote nitayapokea na
uongozi utaangalia kama wanifukuzea au la wao ndio wameniajiwa, kikubwa
ninachoangalia ni uwezo wa wachezaji wangu na zaidi naangalia
mbele."alisema na kuongeza
"Muhimu ni kushinda, haijalishi ni
mechi ya kirafiki au ni Ligi, zinapokutana timu kubwa za watani wa jadi
hakuna mechi raisi, nimejipanga vizuri, lengo ni kushinda, nisingependa
nipoteze."alisisitiza Maximo.
Wakati Maximo akisema hayo, Kocha
wa Simba Patrick Phiri alisema timu yake imeingia Kambini Zanzibar
kujiandaa na mechi ya watani zao Yanga ambao wameshindwa kuwafunga
katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa Oktoba 18, kwa
kutoka suluhu.
Phiri alisema wameanza kujipanga kwa mazoezi
makali ya viungo katika klabu ya mazoezi (gym) ya Chang’ombe, Dar es
Salaam kwa ajili ya kuwajengea nguvu ya mwili wachezaji wake na sasa
wanfanya mazoezi ya uwanjani.
“Mechi inayokuja dhidi yetu na Yanga hakuna droo tena, Simba ni timu kubwa tunahitaji kushinda,” alisema Phiri.
Hata
hivyo matumaini makubwa ya Phiri yapo kwa Dan Sserunkuma kwa kile
alichoeleza mchezaji huyo ni mzuri na amemfuatilia kwa muda mrefu
akiwepo timu ya taifa ya Uganda 'Uganda Crenes' na Gor Mahia.
“Daniel
ni mchezaji mzuri, nimemfuatilia akiwa katika timu yake ya Taifa na
hata akiwa Gor Mahia kule Kenya, huyu ni mshambuliaji aliyekamilika…
naamini atatusaidia sana,” alisema.
" Nataka mashabiki wasihofu
juu ya matokeo ya sasa ya Simba na michezo ya kirafiki badala yake
nitawafurahisha mwaka ujao utakapoanza.
"Kwa sasa nina michezo
miwili migumu iliyobaki mwaka huu, tutacheza na Yanga wikiendi hii kisha
tutavaana na Azam kwenye Ligi Desemba 26 mwaka huu. Mwakani nitakuwa
nimebakiza michezo 18 ili ligi imalizike hivyo ninataka kuhakikisha
ninafanya vizuri na kuchukua ubingwa tena kwa kupata matokeo mazuri.
Hivi
karibuni Simba imecheza michezo miwili ya kirafiki. Mmoja dhidi ya
Express ya Uganda ambao uliisha kwa sare ya 0-0. Kisha wakacheza na
Mtibwa na kupokea kipigo cha 4-2.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...