Wasanii
wa Hip hop katika anga ya muziki wa Bongofleva,Faridi Kubanda a.k.a Fid
Q pamoja na Stamina wakilishambulia jukwaa kwenye tamasha la wazi la
Tuo8January,hapo jana katika viwanja vya sabasaba mjini Morogoro.
Tuo8January ni kampeni maalum iliyozinduliwa hivi karibuni ikiwa na lengo la kuwahamasisha vijana kujitokeza kushiriki mchakato wa
uchaguzi wa viongozi mbalimbali wanaowataka na wanaowaamini wana uwezo
wa kuleta mabadiliko ya kinidhamu kwenye masuala ya msingi ya Taifa
letu.
Kama
vile haitoshi kampeni hiyo inatumika kuwahamasisha vijana wenye uwezo
na sifa za kugombea nafasi za uongozi kuchukua hatua sasa za kufanya
hivyo,pia kupata vijana wen,vijana wenye vigezo vya kupiga kura
pia
ni lazima wafanye hivyo maana ni wajibu wetu na kuwa vijana ni lazima
tushiriki kikamilifu katika mchakato wa kampeni ili kuhakikisha mambo ya
msingi yanajadiliwa na wagombea na yanapewa kipaumbele.
Katika
tamasha hilo Fid Q aliwahamasisha vijana mbalimbali waliojitokeza
kwenye tamasha hilo,kuwa imefika wakati wa vijana kujitokeza kushiriki
mambo mbalimbali ya kimsingi kwa manufaa ya nchi yao na si kukaa chini
na kuanza kulalama,wakati kwenye mambo ya maamuzi wakishirikishwa
hawataki kujitokeza,hivyo ni wakati wao wa kuamka na kuchagua kiongozi
kijana wa kisasa na si kiongozi wa kisiasa.
Msanii
mwingine wa hip hop katika anga ya Bongofleva,ambaye amekuwa akifanya
vyema kwenye muziki huo,Niki wa Pili akitumbuiza katika jukwaa la wazi
la Tuo8Januari lililofanyika mjini Morogoro hapo jana.
Baadhi
ya wakazi wa mji wa Morogoro wakishangilia yaliyokuwa yakijiri kwenye
tamasha la Tuo8January,lililofanyika jana kwenye viwanja vya sabasaba
mjini humo,tamasha hilo la wazi ambalo limewashirikisha wasanii
mbalimbali,ni kampeni maalum ya kuwahamasisha vijana kushiriki katika
chaguzi mbalimbali kwa njia ya matamasha.
Kampeni hiyo ilizinduliwa jijini Dar hivi karibuni
na kufanyika tamasha la kwanza mkoani Njombe na sasa Mkoani
Morogoro.Baadhi ya Wasanii mbalimbali wenye ushawishi mkubwa kwa vijana
wameonesha kuiunga mkono kampeni hiyo,akiwemo Babu Tale, Mwana FA, Nick wa Pili, Lamar, P-Funk, Mwasiti, Barnaba, Ditto,G-nako,Fid Q,Shilole,Yamoto Band,Stamina na wengineo.
Baadhi ya mashabiki wa muziki wa kizazi kipya wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri katika jukwaa la tamasha la Tuo8January,lililofanyika jana katika viwanja vya Sabasaba,mjini Morogoro.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...