Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akilizungumza Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hapo siku ya Alhamis kabla Baraza hilo halijapigia kura Azimio linalotaka kuwapo kwa siku ya Kimataifa ya kuwatambua watu wenye ulemavu wa ngozi. Kulia kwa Balozi ni Bi. Ellen Maduhu Afisa wa Uwakilishi anayeshughulika Kamati ya Tatu inayohusika na masuala ya Haki za Binadamu, Utamaduni na Masuala ya Jamii na alishiriki kikamilifu katika majadiliano ya kwanza kuhusu Azimio hilo ambapo alihakikisha Azimio limetambua juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na kuzikabili changamoto wanazokumbana nazo.
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wakiwa katika mkutano ambao ulipitisha maazimio mbalimbali yaliyowasilishwa mbele ya Baraza hiyo na Kamati ya Tatu. Baadhi ya Maazimio yaliyopitishwa katika mkutano huo uliofanyika siku ya Alhamis lilikuwapo linalopendekeza kuwapo wa siku ya Kimataifa ya watu wenye ulemavu wa ngozi ( Albino).
Na Mwandishi Maalum, New York
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesisitiza kwamba haitoshi kuwa na siku ya kimataifa ya
kuwatambua watu wenye ulemavu wa ngozi ( Albino) pasipo kuwa na mikakati madhubuti
inayolenga katika kuwawezesha.
Hayo yameelezwa na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika
Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi alipokuwa akizungumza muda mfupi kabla ya
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa halijapigia kura Azimio linalotaka kuwepo kwa Siku ya
Kimataifa ya Kuwatambua watu wenye Ulemavu wa ngozi.
Leo ( Alhamsi) Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipokea mapendekezo ya maazimio mbali
mbali yaliyowasilishwa mbele ya Baraza hilo yakitokea Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja
wa Mataifa, Kamati inayohusika na masuala ya Haki za Binadamu, Utamaduni na Maendeleo ya
Jamii.
Miongoni mwa Maazimio hayo lipo lililohusiana na Haki za Binadamu ambapo ndani ya
maazimio ya eneo hilo kuna azimio linalopendekea kuwa wa siku ya kimataifa ya watu
wenye ulemavu wa ngozi.
Balozi Manongi amelieleza Baraza hilo kuwa, kimsingi Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
haipingi kuwapo kwa siku ya kimataita ya kuwatambua watu wenye ulemavu wa ngozi . Lakini
inapata shida pale azimio hilo linaposhindwa kuainisha mchango na mikakati ya kimataifa ya
kuwezesha jamii hiyo kukabiliana na changamoto mbalimbali.
Akiongea kwa msisitizo, Balozi Tuvako Manongi ameeleza kuwa Tanzania ni nchi ambayo
inaidadi kubwa ya watu wenye ulemavu wa ngozia na pamoja na changamoto na matatizo
wanayokumbana nayo.
Amezitaja baadi ya changamoto hizo na ambazo pia zimeainishwa katika Tume ya Haki za
Binadamu kuwa ni pamoja na kutopata huduma kamilifu za kiafya, elimu, kunyanyapaliwa na
madhira mengine.
“Kuna changamoto mbalimbali zinazowakabili, Changamoto ambazo zinatakiwa kufanyiwa
kazi na kutafutiwa ufumbuzi. Kama nchi yenye idadi kubwa ya watu wenye ulemavu wa ngozi,
Ujumbe wangu ulijjitahidi katika kuhakikisha kuwa pendekezo la Azimio hili ambalo leo
limeletwa mbele ya Baraza hili linakuwa lenye tija na manufaa zaidi kwa walengwa kuliko lilivyo
hivi sasa” amesema Balozi Manongi
Amesema kuwa pamoja na kwamba pendekezo hilo la kuwa na siku ya kimataifa ya watu
wenye ulemavu wa ngozi ni hatua muafaka, lakini halitoi mwelekeo wa namna ya kushughulikia
matatizo yao pamoja na uwezeshwaji wao.
Ni kwa sababu hiyo na kutokana na mapungufu hayo ambayo yalikuwa hayatoi nafasi wa
Jumuiya ya Kimataifa kushirikiana na Juhudi za Tanzania katika kuzikabili changamoto
zinazowakabili watu wenye ulamemavu wa ngozi.Ndiyo maana Tanzania kwa nia njema kabisa
iliomba azimio hilo lipigiwe kura si kwa maana ya kulipinga azimio lakini kupinga azimio hilo
kutokuwa na maslahi mapana kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.
Mwakilishi huyo wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, amekwenda mbali zaidi kwa kusema
kuwa Tanzania na kama ilivyokuwa kwa wanachama wengine, imekuwa ikiaamini kuwa
Chombo hicho kwa maana ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na Umoja wa Mataifa kwa
ujumla wake vinapashwa kupitisha maamuzi na maazimio yenye tija zaidi.
Azimio hilo limepitishwa kwa kupigiwa kura ambapo licha ya mapungufu yake, inatambua
kuwa June 16 ya kila mwaka itakuwa ni siku ya Kimataifa ya kuwatambua watu wenye
ulemavu wa ngozi (Albino)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...