DSC_0202
Afisa Ardhi na Mazingira wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala (Kahama), Zablon Donge, akifungua rasmi warsha ya siku tatu ya wadau wa mapambano dhidi ya UKIMWI kwa niaba ya Mkurugenzi wa wilaya hiyo, iliyofanyika Kata ya Segese wilayani Kahama mkoani Shinyanga. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues pamoja na Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias.

Na Mwandishi Wetu, Kahama
MKURUGENZI Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues ametaka jamii kujumuisha suala la utamaduni katika kupambana na maambukizi mapya ya Ukimwi.

Alisema hayo kwenye warsha ya siku tatu ya wadau wa mapambano dhidi ya UKIMWI inayofanyika Kata ya Segese wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Alisema katika ufunguzi huo kwamba kwa miaka mingi pamoja na kuwepo kwa elimu ya UKIMWI, kumekosekana mabadiliko yanayotakiwa kukabili maambukizi mapya.

Alisema UNESCO iliangalia tatizo hili na kubaini kwamba kutobadilika kwa hali kumetokana na kutounganishwa kwa kipengele cha mila ambacho ndicho kinachofanya kuwepo na mazingira rafiki ya kupashana habari.
DSC_0151
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akizungumza na washiriki wakati wa uzinduzi wa program ya utamaduni kukabili UKIMWI itakayoendeshwa na shirika lake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...