Washiriki Kumi na Wanne (14) kutoka Tanzania wajumuika na wenzao 20 kutoka nchi mbalimbali za Afrika katika Maonyesho ya Pili Sekta ya Afya chini Uturuki. Maonyesho hayo hufanyika kila mwaka na kwa lengo la kuendeleza mahusiano na ushirikiano katika kuboresha Sekta ya Afya kwa nchi husika. Maonyesho ya Mwaka huu yalikuwa na washiriki kutoka nchi 60 duniani kote.  Kwa upande wa Afrika mkutano huu ulioratibiwa na kusimamiwa na kampuni ya kuendeleza mahusiano ya maendeleo na biashara kati ya Afrika na Uturuki iitwayo TurkaAfrica Ltd (www.turkafrica.co.tz).
  Waandaaji wa TurkAfrica wakiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wao TUSMSIAD,na Washiriki kutoka Tanzania.
 Waziri wa Afya Zanzibar Mh. Rashid Seif Suleiman akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Afya wa Uturuki Hon. Mehmet Müezzinoğlu. Kushoto ni Dr. Lulu Fundikira (kutoka Hopitali ya Taifa Muhimbili) akifuatiwa na Mshauri wa mambo ya Uchumi na Maendeleo wa Serikali ya Uturuki ambaye pia ni Raisi wa Taasisi ya Uchumi na Biashara ya Uturuki (TUMSIAD) – Dr. Hassan Sert. Kulia ni Jumanne Simba.
 Waziri wa Afya Zanzibar Mh. Rashid Seif Suleiman akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa sekta ya Afya wa Serikali ya Uturuki mara baada ya mazungumzo ya njia mbalimbali za kuboresha sekta ya Afya na mahusiano kati ya Serikali ya Uturuki na Tanzania.
 Waziri wa Afya Zanzibar Mh. Rashid Seif Suleiman akifanya mazungumzo na Waziri wa Afya wa Uturuki Hon. Mehmet Müezzinoğlu. Kushoto ni Dr. Athuman Ngenya na washiriki wengine kutoka Tanzania. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongereni sana Turk Africa haya ndiyo maendeleo yanayotakiwa kuletwa Tanzania na Africa kwa ujumla.

    Mdau - Mzalendo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...