Naibu Waziri wa Maji,Mh Amos Makala amewataka wananchi wa Mkoa wa Arusha kuendelea kuwafichua wale wote wanaoshiriki katika wizi wa maji ili waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.Alitoa wito huo jana wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi jijini hapa kwa lengo la kutembelea miradi ya maji iliyokuwa na changamoto kubwa ya upotevu wa maji inayosababishwa na uchakavu wa miundombinu na wizi wa maji

Waziri Makala alisema kuwa serikali inafanya jitihada ya kuboresha huduma ya maji ikiwa nipamoja na kuboresha miundombinu,kukomesha wizi wa maji kwa kutoa elimu kwa wananchi.“Wizi wa kujiunganishia maji katika maeneo mbalimbali hapa nchini upo lakini kwa sasa tunaoparesheni ya kuwasaka wale wote wanaotumia maji bila kulipa watambue kuwa kwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria”alisema Makala

Aidha katika moja ya chanzo kikubwa cha maji mto nduruma alisema kuwa chanzo hicho kinategemewa kwa mkoa wa Arusha hivyo alitoa pongezi kwa mamlaka ya maji kwa kuwa wabunifu.
Naye Kaimu mkurugenzi wa mamlaka ya maji Arusha Eng.Fabian Maganga alisema kuwa kwa hivi karibuni walikuwa na zoezi la ukaguzi wa nyumba hadi nyumba na kufanikiwa kuwakamata watu wanaohujumu mamlaka hiyo takribani 750 hivyo zoezi hilo bado ni endelevu.
SAM_0190Naibu Waziri wa Maji,Mh Amos Makala akiongea na vyombo vya habaria katika ziara yake ya kikazi jijini hapa kwa lengo la kutembelea miradi ya maji iliyokuwa na changamoto kubwa ya upotevu wa maji inayosababishwa na uchakavu wa miundombinu na wizi wa maji
SAM_0188
 Naibu Waziri wa Maji,Mh Amos Makala kulia akiwa anasikiliza maelezo kutoka kwa Eng wa maji Bw.Mohamed Ismail katika eneo la chanzo cha maji mto nduruma katikati niKaimu mkurugenzi wa mamlaka ya maji Arusha Eng.Fabian Maganga 
SAM_0178

Muonekano wa maporomoko ya maji mto nduruma ni chanzo kikubwa kinachotegemewa Mkoani Arusha katika huduma ya maji
SAM_0191
Askari anayelinda eneo hilo.Na Pamela Mollel wa jamiiblog.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tuanze kwanza na wezi wa ESCROW.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...