Balozi wa China nchini Tanzania,LU Youqing akicheza ngoma ya asili ya Mkoa wa Kagera wakati alipokuwa akilakiwa kwenye uwanja wa ndege wa Bukoba.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera, John Mongella .
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, John Mongella akimkabidhi Balozi wa China nchini Tanzania,LU Youqing Hati na ramani eneo lililotengwa na serikali ya mkoa kwa ajili ya kujenga chuo cha Ufundi (VETA) cha Kitaifa kilichoahidiwa na serikali ya China wakati wa ziara ya Rais Kikwete nchini humo mwaka jana. 
Balozi wa China nchini Tanzania,LU Youqing akipokea zawadi ya ramani ya Afrika Mashari iliyochorwa kutoka kwa wanafunzi wa shule ya Mgeza Mseto. 

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Aise Bukoba pazuri saaaaaaaaaaaana!! Karibuni ambao hamjawahi kufika huko!!

    ReplyDelete
  2. Hicho chuo cha Veta kikijengwa kitainua mkoa huo ambao uko pembezoni lakini una mandhari nzuri hasa maeneo yanayopakana na ziwa viktoria. Walio na uwezo wa kuwekeza nao wafikirie kufanya hivyo ili mkoa uendelee mbele.

    ReplyDelete
  3. safari hii hajavishwa kofia ya ccm?

    ReplyDelete
  4. Ukitaka vya uvunguni sharti uiname.Wachina wanajua nini wanataka, ndiyo maana babu balozi anakatika na midundo ya kina waitu.

    ReplyDelete
  5. Ukiangalia majengo mazuri pale mjini katikati yaliyochukuliwa na shirika la nyumba yameandikwa kwamba yalijengwa mwaka 1956, hii inaonyesha utaifishaji usingesababisha uzorotaji wa kuendeleza miji mikoa ingekuwa imejengeka sana. Fursa zipo za kuendeleza miji hata watu binafsi wathubutu kuwekeza majengo ya vitega uchumi kuendeleza mikoani na wilayani

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...